Friday, 18 March 2016

SHAHIDI ATINGA MAHAKAMAI NA MASUFURIA



SHAHIDI wa tatu wa mlalamikaji, James Lembeli katika kesi ya kupinga matokeo ya ubunge yaliyompa ushindi Mbunge wa Jimbo la Kahama Mjini, Jumanne Kishimba (CCM) jana alitinga Mahakama Kuu Kanda ya Shinyanga akiwa na mzigo wa masufuria, akidai alipewa kwa ajili ya kumpigia mgombea ubunge wa CCM. ..,





Mbele ya Jaji Moses Mzuna anayesikiliza shauri hilo, Cesilia Gregory wa Nyahanga mjini Kahama alikiri kupokea zawadi ya masufuria hayo kutoka kwa Wakala wa Kishimba ili ampigie kura.

Gregory alidai Oktoba 19, 2015, Kikundi cha Amani waliitwa nyumbani kwa Hamad Hilal na kumkuta Ezra Machogu, ambaye alikuwa ni Wakala wa Kishimba akigawa masufuria yalitolewa kwa ajili ya kumuombea kura mgombea ubunge wa CCM.

Hata hivyo, kulitokea mvutano baada ya Wakili wa Kishimba, Antony Nansimire kumtaka shahidi kuwataja wanakikundi 20 ambao walipewa masufuria hayo, hivyo kuwataja 22 na kwamba ongezeko hilo lilisababishwa na baadhi ya wanaume waliojiunga kuhamasisha utafutaji wapiga kura wa Kishimba.

Wakati huohuo, mawakili wa mdai katika shauri la kupinga matokeo ya ubunge Jimbo la Kyerwa mkoani Kagera, Benedicto Mutungirehi wamejitoa.

Hatua hiyo ilifuatia makosa ya kisheria yaliyobainishwa katika hati ya kiapo cha shahidi wa pili, Pastory Bagambila ambaye tayari alikuwa mbele ya Mahakama kutoa ushahidi wake.

Baada ya kubaini makosa hayo, Wakili Erasto aliiomba Mahakama kumuondoa shahidi huyo kutoka kwenye orodha ya mashahidi kabla ya kutoa ombi la kujadiliana kwa muda na mteja wake.

Hata shahidi wa tatu, Alistides Boniface alipoitwa naye hati yake ya kiapo ilibainika kuwa na kasoro za kisheria, hali iliyomtia hofu Wakili Erasto kuwa yawezekana viapo vya mashahidi wote 36 vilivyowasilishwa vina kasoro.

Kabla ya kujitoa, wakili Erasto alimuomba Jaji Maisario Munisi anayesikiliza shauri hilo, kuahirisha kwa muda ili wajadiliane na mteja wao.

Waliporejea mahakamani baada ya dakika 30, Wakili Erasto alimweleza Jaji Munisi kuwa wanaomba kujitoa kwa maelekezo ya mteja wao.

Kutokana na hali hiyo, Mutungirehi aliiomba Mahakama kumpa muda kutafuta wakili, ombi lililokubaliwa na Jaji Munisi na kuiahirisha hadi Machi 22.

Mbunge wa sasa wa jimbo hilo kupitia CCM, Innocent Bilakwate anawakilishwa na Wakili Peter Matete.

Baadhi ya maombi yake ya msingi, Mutungurehi anadai kulikuwapo na ukiukwaji sheria, taratibu na kanuni katika kuhesabu kura na kudai kulitawaliwa na usiri bila kumhusisha.


NAFASI KIBAO ZA KAZI DAR ES SALAAM


Job Description

DAR ES SALAAM MARITIME INSTITUTE (DMI)
EMPLOYMENT OPPORTUNITY

Dar es Salaam Maritime Institute (DMI) invites qualified Tanzanians with relevant qualifications to apply for the positions as spelt out hereunder.

1. Senior Lecturer
2. Lecturer
3. Assistant Lecturer
4. Assistant Tutor/ Instructor
5. Principle Administrative and Personnel Officer
6. Administrative & Personnel Officer
7. Senior Accountant
8. Accountant
9. Internal Auditor
10. Librarian
11. Supplier Officer
12. Record Management Assistant
13. Secretary II
14. Driver

Mode of Application
i) Application letters ii) Curriculum Vitae iii) Certified copies of academic/professional certificates iv) Mobile phone number and email address v) Names of three referees

Application should be marked on top of envelop with tittle of the position you are applying for, and should reach the postal address indicated below within two(2) weeks from the date of this advertisement.
Only shortlisted candidates will be contacted

N.B
i) All applicants should be Tanzanian citizens and not above 45 years of age
ii) All certificates from foreign examination bodies should be verified by relevant authorities
iii) All applications should be directed to the:

Principal,
Dar es Salaam Maritime Institute,
P.O. Box 6727
Dar es Salaam

Source: Mwananchi March 17, 2016



- See more at: http://www.vijanatz.com/tz/jobs/?job_listing=senior-lecturer-lecturer-assistant-lecturer-assistant-tutor-instructor-principle-administrative-and-personnel-officer-administrative-personnel-officer-senior-accountant-accountant-internal#sthash.Me2c3J8V.dpuf

MSTAHIKI MEYA WA MANISPAA YA ILALA ALIVYODHALILISHWA NA SERIKALI YA MAGUFUL

I

Makamanda pipozzzzz! Jana nilipokea mwaliko wa maneno kutoka kwa Mkuu wa Wilaya kupitia kwa Mkurugenzi wangu Manispaa ya Ilala wakinitaka niungane nao leo (jana) kwenye ziara ya Raisi Kinýerezi kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa kituo kipya cha kufua umeme wa gesi na mvuke 240 MW (Kinyerezi II), mradi unaotarajiwa kukamilika 2018.

Nilipofika nilipokelewa na kiongozi mmoja wa protocal ambaye ananifahamu kwa kuwa tulikuwa tunasali pamoja zamani akanikabidhi kwa public relation manager wa Tanesco ambaye pia ananifahamu tangu akiwa mwandishi wa habari na mimi nikiwa mwanaharakati wa kupinga wawekezaji wa TTCL.

Kama Meya nilipangiwa kukaa jukwaa kuu la Raisi kati ya matatu ambayo mengine yalikaliwa na waheshimiwa wabunge na wawekezaji, lingine likikaliwa na wakurugenzi na viongozi wengine.

Sasa kituko kikaanza, Mkurugenzi mkuu wa Tanesco akaanza kutambulisha watu walio ktk jukwaa kuu akataja karibu wote pamoja na mbunge Bona aliyekaa pamoja na mimi kwa heshima ya mbunge mwenyeji akaniruka mimi japokuwa alikwishaambiwa uwepo wangu!

Baadae alimkaribisha Raisi aliyekuja na kituko cha mwaka. Aliendelea kutambulisha mabalozi na wawekezaji, mkewe, mbunge Zungu (Ilala), mbunge Kessy (Nkasi Kaskazini) akamruka Anatropia wa CDM, akamwita mbele mbunge Bona na kumsifia sana akisema kwamba wananchi wa Segerea walifanya vizuri kuchagua mbunge wa ccm kama na yeye alivyo wa ccm na kwamba kwa kufanya hivyo watapata maendeleo kwa sababu ati hawezi kumpa mtoto wa jirani chakula wakati wakwake yupo!

Kama hiyo haikutosha akampa nafasi ya kusalimia wananchi! Haikuishia hapo akasema amemchagua mkuu wa mkoa Makonda kwa vile ni mchapakazi na kwamba wengine walikuwa wakigombana naye na kujidai kukataa fedha za maendeleo sasa yeye kampa ukuu wa mkoa awe bosi wao sasa aone kitakachoendelea!

Kauli hii iliniacha hoi. Kama vile haitoshi akasema tena kwamba amemteua mchapakazi mwingine ambaye wasiopenda maendeleo wanampinga Mh. Muhongo. Ati naye atawakomesha wale waliokuwa wanapenda kukodishakodisha mitambo ya kufua umeme. Ati anampongeza kwa kuvunja bodi iliyokuwa inamshauri kukodishakodisha mitambo ya ajabuajabu.

Yote hiyo ni mipasho kwa wapinzani ambayo haikutakiwa kutoka kwenye kinywa cha Raisi. Ile ilikuwa ziara ya kiserikali siyo ya chama chake. Na madongo mengine mengi kawarushia wapinzani utafikiri akina mama wanaocharurana kwa mafumbo.

Nimejuta kwenda huko na sitakaa niende tena kwenye ziara zake kwani huko ni kufuata maudhi badala ya kufurahia maendeleo ambayo ndiyo lengo la UKAWA.

TAMKO ZITO LA WAKRISTU ZANZIBAR

Jukwaa la Wakristo Tanzania (TCF) limetoa tamko kuhusiana na hali ilivyo sasa Zanzibar likisema linafadhaishwa na kusikitishwa nayo na kwamba linaamini isingefikia hapo endapo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ingechukua hatua katika kutatua mgogoro huo.

Katika tamko hilo lililosambazwa kwenye vyombo vya habari jana baada ya kikao cha TCF juzi, yamo mapendekezo manne likiwamo la kuitaka Serikali kurejesha mchakato wa Katiba kwa kuzingatia maudhui yaliyomo katika Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba ili kuondoa utata wa Serikali kushiriki masuala ya Zanzibar.

“Sisi viongozi wa dini tuliokutana leo tarehe 15.03.2016, tunafadhaishwa na kusikitishwa na hali ya Zanzibar kwa sasa.

"Hali ya Zanzibar isingefika hapo ilipo iwapo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ingechukua hatua ya kutatua mgogoro huu.

"Hali hii ya Zanzibar na udhaifu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano vinapelekea kushindwa kwa Serikali ya Muungano kuchukua hatua ya kusaidia hali ya Zanzibar. Hata hivyo, udhaifu huu wa Katiba hauondoi wajibu wa Serikali ya Muungano kuhakikisha haki na amani vinatawala Zanzibar,” ilisema sehemu ta tamko hilo lililotiwa saini na Askofu Mkuu wa Dayosisi ya Mwanza, Jude Ruwa’ichi.

Jukwaa halikufafanua hali ya Zanzibar kwa sasa inay- osababisha maaskofu hao kufadhaika lakini huenda limekusudia kueleza hofu iliyotanda katika visiwa hivyo tangu Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) ilipofuta uchaguzi na matokeo yote ya uchaguzi wa Zanzibar, na baadaye kutangaza kuwa utarudiwa Machi 20.

Vyama tisa kikiwamo Chama cha Wananchi (CUF) vilitangaza kujitoa lakini ZEC imesisitiza vyama vyote vitashiriki.

Hali imeendelea kuwa tete na hivi karibuni yamekuwapo matukio ya uchomaji moto makazi ya watu katika visiwa hivyo yanayoonyesha uvunjifu wa amani kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi wa marudio Jumapili ijayo.

Baadhi ya matukio hayo ni kuchomwa moto maskani za CCM na CUF, nyumba 11 za watu ikiwamo ya Kamishna wa Polisi Zanzibar, Hamdan Omar Makame iliyoko Kijichi, Mkoa wa Mjini Magharibi.

Baada ya kutathimini hali hiyo, TCF imesema pamoja na udhaifu wa Katiba, Serikali ya Muungano bado ina wajibu wa kuhakikisha uhuru, haki na amani vinatawala Zanzibar kuelekea uchaguzi huo wa marudio.

“Hata hivyo, Serikali ya Muungano pamoja na taasisi zinazosimamia mchakato wa uchaguzi, zinao wajibu wa kuhakikisha kuwa suala la uhuru, haki na amani Zanzibar vinalindwa na kuheshimiwa. Suala la uhuru, haki ni wajibu wetu sisi viongozi wa dini na Watanzania wote na halina mbadala,” ilisema sehemu ya tamko hilo.

Jukwaa limesisitiza kwamba ni jukumu la kila mmoja kutimiza wajibu wake kulinda uhuru, haki na amani na kuweka uzalendo kwanza kuliko kutanguliza maslahi binafsi au ya vyama vya siasa.

Mbali ya pendekezo la kuitaka Serikali kurejesha mchakato wa Katiba, pia limewataka viongozi wa dini kuwahimiza Watanzania wote kuendelea kuiombea Tanzania (Bara na Zanzibar) ibaki kuwa Taifa lililojengwa katika msingi ya uhuru, haki na amani.

Pili, limelitaka Jeshi la Polisi, vikosi vya ulinzi na usalama na Jeshi la Wananchi wa Tanzania, kwa wakati huu kuendelea kutimiza wajibu wa kusimamia amani na taratibu kwa haki bila upendeleo.

Mwisho limesisitiza kwamba viongozi wa dini wabaki kuwa sauti ya kinabii na wahubiri wa uhuru, haki na amani wakati huu, wakati wa uchaguzi na haada ya uchaguzi.

Thursday, 17 March 2016

HISIA HIZI NI HATARI KATIKA MAPENZI

Miongoni mwa vitu vinavyochangia kuharibu uhusiano wa kimapenzi ni hisia. Wapenzi wengi wameachana kwa sababu si kwamba walithibitisha ubaya wa wenzao ila walijijaza wenyewe hisia mbaya na kujikuta wamepoteza thamani ya kupenda. Hebu angalia hisia nane hatari ili uzikimbie mapema kabla hazijakuharibia penzi lako. 

1. NASALITIWA

Kuishi katika mapenzi huku ukiwa na fikra kwamba mwenza wako anakusaliti ni jambo baya kwa vile huathiri msukumo wa ndani wa kupenda. Matokeo yake utajikuta ukishindwa kutimiza wajibu wako kama mke/mume kwa sababu tu ya kuendekeza hisia mbaya. Acha kuhisi, tafuta ukweli.

2. TUTAACHANA
Kuna wapenzi ambao wanaishi na mawazo ya “ipo siku tutaachana”. Wanafanya hivyo eti kwa kutafsiri mwenendo usioridhisha wa mapenzi yao. Kusema kweli hili ni jambo baya kwani huondoa ari na kujenga ufa wa mapenzi. Huwafanya wapenzi kubakia na wazo moja tu, la kutafuta sehemu mbadala ya kwenda baada ya kuachana. Usiwaze kabisa kuachana hata kama mnagombana na mwenzako kila siku.

3. SIWEZI MAPENZI
Baadhi ya wapenzi huwa na hisia kwamba hawayawezi mapenzi. Hata kama hawajaambiwa chochote kuhusu kutowatosheleza wenza wao faragha hukimbilia kujihukumu. Hujaambiwa kama umecheza chini ya kiwango, hofu ya nini? Usiwaze hivyo, kama una lolote linalokufanya uwe na hofu muulize mwenzio.

4. NINA KASORO
Naamini mitaani wapo watu ambao huamini wana kasoro fulani ndiyo maana hawafikii viwango vya kupendwa kama wanavyovihitaji. “Yaani mimi ningekuwa kama fulani ningefurahi sana lakini ufupi wangu ndiyo tatizo.” Hizi ni hisia mbaya tu, kumbuka kuna wafupi wanapendwa ile mbaya. Jisahihishe na epuka kujishusha hadhi kwenye hisia zako.

5. NITAMUUA
Miongoni mwa hisia mbaya kabisa kwenye mapenzi ni kufikiria kumuua mwenzako kwa sababu yoyote. “Nikimfumania na mwanaume mwingine nitamuua.” Mtu anayetawaliwa na mawazo ya aina hii anajiweka katika mtego mbaya kisaikolojia wa kuja kutekeleza kile anachojiapiza hata kwa sababu ndogo. Usifikirie hivyo maishani mwako.

6. NIMEKOSEA KUCHAGUA
Usijihukumu makosa kwa sababu umeona mpenzi wako ana tatizo fulani. Fahamu kuwa kasoro ni sehemu ya ubinadamu. Weka mikakati ya kumuongoza mwezio kuliko kuhitimisha kwa mawazo kwamba ulikosea kumchagua. “Ningejua kama yuko hivi nisingemchagua.” Usiwaze hivi!


7. HATUWEZI KUZAA
Kuna wapenzi ambao kwa kuishi miaka mitatu au minne pamoja bila kupata mtoto hufikia kwenye fikra kwamba hawawezi kuzaa. “Mmm, mwaka wa nne umepita bila mtoto, nadhani sisi hatuwezi kuzaa.” Kwa nini msizae?Hizo ni fikra zako, hamjaambiwa na daktari sasa iweje uwaze hivyo? Jipe moyo kwani kuna watu walizaa baada ya miaka kumi, iweje ninyi wa mwaka mmoja?

8. UNANIDANGANYA
Ipo aina ya watu ambao hata kama wakiambiwa wanapendwa sana, hukimbilia kusema na kuamini kuwa wanadanganywa. “Mmm unanidanganya.” Atasema hivyo licha ya kuona mwanaume anavyojituma kumsotea na kumuonesha kila dalili za mapenzi. Hili ni jambo baya, ukithibitisha kwamba unapendwa usihisi unadanganywa, utapoteza bahati yako.


Wednesday, 16 March 2016

MENGI BLAMES AFRICAN GOVERNMENTS



Kwa tafsiri ya kawaida ya kiswahili " Baadhi ya viongozi wa Africa wanatengeneza mazingira magumu ya kibiashara halafu wanawalaumu wananchi kuwa hawawezi kufanya biashara"...Reginald Mengi.

EMPLOYMENT OPPORTUNITIES

International Organization for Migration


Open to Internal and External Candidates

Position Title : IT Assistant ( 1 Position)
Duty Station : Kigoma Region
Classification : General Service Staff, Grade G4
Type of Appointment : Ninemonths, with possibility of extension
Estimated Start Date : As soon as possible

Closing Date : March 28th, 2016


Established in 1951, IOM is the leading inter-governmental organization in the field of migration and works closely with governmental, intergovernmental and non-governmental partners. IOM is dedicated to promoting humane and orderly migration for the benefit of all. It does so by providing services and advice to governments and migrants.

IOM is committed to a diverse and inclusive environment. Internal and external candidates are eligible to apply to this vacancy. For the purpose of the vacancy, internal candidates are considered as first-tier candidates.

Context:

Under the overall supervision of the Head of Sub Office and the direct supervision of the Resource Management Officer and in coordination Admin/Finance Unit the incumbent will carry out the following duties and responsibilities:

Core Functions / Responsibilities:

1. Setup and maintain the IT equipment for the users in office. 
2. Install and maintain Internet connections for Kigoma office. 
3. Install and administer the security for various system and network components, including access to internet, protection against viruses, etc. 
4. Provide the user support for MS Windows, and MS Office, as well as for other programs used in the office.
5. Analyze computer systems; recommend new systems and/or enhancements in the functionality of the existing systems. 
6. Implement the proper backup/restore, data validation and security procedures to assure data integrity and availability.
7. Identify and support technology solutions for database related support.
8. Assist in administration of Database Server and fixing of database related problems.
9. Run Database queries and procedures
10. Assist in maintenance of systems, sub systems and modules of mission database in accordance with the needs and requirements of each program and project. 
11. Provide user support, and training to use, operation, and maintenance of the databases and assist in the implementation of all auxiliary sub systems and modules. 
12. Other related duties as required. 

Required Qualifications and Experience

Education

• University Degree in IT, Computer Science or related field; or an equivalent combination of education, training and experience
• Minimum 4 years’ experience 
• Knowledge of Microsoft Operating Systems, Server Administration, Networking and Desktop applications and Databases
• Knowledge in TCP/IP Networking 
• Knowledge of LAN/WAN Technologies
• Experience in the following tools: MS SQL Server, C++, MS Access is a plus
• Any certification is a plus: CCNA

Experience 
• Demonstrated ability to maintain accuracy and confidentiality in performing responsibilities.
• Previous work experience with an international organization and NGOs dealing with refugees would be a strong advantage

Languages

Fluency in English and Kiswahili is required. 

Required Competencies

Behavioural 

• Accountability – takes responsibility for action and manages constructive criticisms
• Client Orientation – works effectively well with client and stakeholders
• Continuous Learning – promotes continuous learning for self and others
• Communication – listens and communicates clearly, adapting delivery to the audience
• Creativity and Initiative – actively seeks new ways of improving programmes or services
• Leadership and Negotiation – develops effective partnerships with internal and external stakeholders;
• Performance Management – identify ways and implement actions to improve performance of self and others.
• Planning and Organizing - plans work, anticipates risks, and sets goals within area of responsibility;
• Professionalism - displays mastery of subject matter
• Teamwork – contributes to a collegial team environment; incorporates gender related needs, perspectives, concerns and promotes equal gender participation.
• Technological Awareness - displays awareness of relevant technological solutions;
• Resource Mobilization - works with internal and external stakeholders to meet resource needs of IOM.

Other

Any offer made to the candidate in relation to this vacancy notice is subject to funding confirmation. 

Appointment will be subject to certification that the candidate is medically fit for appointment and verification of residency, visa and authorizations by the concerned Government, where applicable.

Only candidates residing in either the country of the duty station or from a location in a neighbouring country that is within commuting distance of the duty station will be considered. In all cases, a prerequisite for taking up the position is legal residency in the country of the duty station, or in the neighbouring country located within commuting distance, and work permit, as applicable.

How to apply:

Interested candidates should fill in the PH form, submit CV and cover letter indicating Vacancy Notice number with 3 professional references and contacts to tzvacancy@iom.int

Or send applications to the address below;

International Organization for Migration Mission in the United Republic of Tanzania
Slipway Road, off Chole Road, Plot # 1365 Msasani. PO Box 9270 Dar es Salaam, Tanzania

Kindly note only shortlisted candidates will be contacted. 
For further information, please refer to: https://tanzania.iom.int/

Posting period:

From 15.03.2016 to 28.03.2016
===========



Open to Internal and External Candidates

Position Title : Laboratory Clerk ( 1 Position)
Duty Station : Kigoma Region
Classification : General Service Staff, Grade G3
Type of Appointment : Ninemonths, with possibility of extension
Estimated Start Date : As soon as possible

Closing Date : March 28th, 2016


Established in 1951, IOM is the leading inter-governmental organization in the field of migration and works closely with governmental, intergovernmental and non-governmental partners. IOM is dedicated to promoting humane and orderly migration for the benefit of all. It does so by providing services and advice to governments and migrants.

IOM is committed to a diverse and inclusive environment. Internal and external candidates are eligible to apply to this vacancy. For the purpose of the vacancy, internal candidates are considered as first-tier candidates.
Context:

Under the overall supervision of the Chief Medical Officer, the direct supervision of the National Migration Health Physician in coordination with the Regional Laboratory Specialist the incumbent will carry out the following duties and responsibilities:

Core Functions / Responsibilities:

1. Assist in the collection and processing of sputum specimens for testing in migration related health assessments. 
2. Prepare specimens and arrange transport for follow-up testing as required.
3. Strictly follow all anti-fraud measures for specimen collection
4. Perform serological testing for the migration health programs including both screen and confirmatory testing
5. Carry out the sterilization processes for the laboratory reagents and waste disposal
6. Timely process of laboratory specimens and result posting, including Pre-Departure Medical Screening result posting.
7. Strictly follow all safety guidelines and instructions including the use of PPE.
8. Strictly follow all Standard Operating Procedures SOP’s for testing conducted
9. Liaise with the Regional Laboratory Specialist in order to monitor quality assurance measures for the collection and testing of all specimens according to IOM guidelines and inform supervisor of any discrepancy.
10. Maintain an electronic database for all IOM laboratory testing.
11. Perform any other duties that may be assigned by from time to time.

Required Qualifications and Experience

Education

• Diploma in Medical Laboratory Techniques (Registered in Tanzania) 
• Minimum of three years’ work experience in a Medical Laboratory environment
Experience 
• Training and experience in TB, HIV, STDs and other communicable diseases testing 
• Mature individual, able to work independently, effectively and harmoniously with colleagues from varied cultures and professional backgrounds at all levels
• Tolerant individual with ability to work with migrants at all ages and from different background and with flexibility and able to work on overtime, when requested
• 
• Capable of working under stressful and difficult conditions
• Demonstrated ability to maintain accuracy and confidentiality in performing responsibilities.
• Previous work experience with an international organization and NGOs dealing with refugees would be a strong advantage
• Proficiency in computer skills, especially in MS Office (Excel, Word, Access) and experience in working with databases and online applications

Languages

Fluency in English and Kiswahili is required. 

Required Competencies

Behavioural 

• Accountability – takes responsibility for action and manages constructive criticisms
• Client Orientation – works effectively well with client and stakeholders
• Continuous Learning – promotes continuous learning for self and others
• Communication – listens and communicates clearly, adapting delivery to the audience
• Creativity and Initiative – actively seeks new ways of improving programmes or services
• Leadership and Negotiation – develops effective partnerships with internal and external stakeholders;
• Performance Management – identify ways and implement actions to improve performance of self and others.
• Planning and Organizing - plans work, anticipates risks, and sets goals within area of responsibility;
• Professionalism - displays mastery of subject matter
• Teamwork – contributes to a collegial team environment; incorporates gender related needs, perspectives, concerns and promotes equal gender participation.
• Technological Awareness - displays awareness of relevant technological solutions;
• Resource Mobilization - works with internal and external stakeholders to meet resource needs of IOM.

Other

Any offer made to the candidate in relation to this vacancy notice is subject to funding confirmation. 

Appointment will be subject to certification that the candidate is medically fit for appointment and verification of residency, visa and authorizations by the concerned Government, where applicable.

Only candidates residing in either the country of the duty station or from a location in a neighbouring country that is within commuting distance of the duty station will be considered. In all cases, a prerequisite for taking up the position is legal residency in the country of the duty station, or in the neighbouring country located within commuting distance, and work permit, as applicable.



How to apply:

Interested candidates should fill in the PH form, submit CV and cover letter indicating Vacancy Notice number with 3 professional references and contacts to tzvacancy@iom.int

Or send applications to the address below;

International Organization for Migration Mission in the United Republic of Tanzania
Slipway Road, off Chole Road, Plot # 1365 Msasani. PO Box 9270 Dar es Salaam, Tanzania

Kindly note only shortlisted candidates will be contacted. 
For further information, please refer to: https://tanzania.iom.int/

Posting period:

From 15.03.2016 to 28.03.2016
=============

NURSE (2 POSTS) 

POSITION DESCRIPTION:

Under the overall supervision of the Chief Medical Officer in Kigoma, direct supervision of Medical Health Officer and in coordination with the National Medical Officer, the incumbent will be responsible for assisting in performing required routine clinical tasks/procedures in connection with the health assessment and treatment to ensure that identified refugees and migrants are medically fit to migrate in accordance with the medical/health requirements of the receiving countries.


APPLICATION INSTRUCTIONS:

Interested candidates should fill in the PH form(https://tanzania.iom.int/vacancies), submit CV and cover letter indicating Vacancy Notice number with 3 professional references and contacts thru tzvacancy@iom.int

Or send applications to the address below;

International Organization for Migration Mission in the United Republic of Tanzania
Slipway Road, off Chole Road, Plot # 1365 Msasani. PO Box 9270 Dar es Salaam, Tanzania

Kindly note only shortlisted candidates will be contacted.
For further information, please refer to: https://tanzania.iom.int/
=============

OPERATIONS ASSISTANT (5 POSTS) 

POSITION DESCRIPTION:

Under the overall supervision of the Resource Management Officer and direct supervision of the Procurement and Logistics Officer in Kigoma, the incumbent will be responsible for implementing the activities of the operations unit, coordinating and communicating daily activities of the Transit Centre (TC) with other units and partner agencies in the Transit Centre. 

APPLICATION INSTRUCTIONS:

nterested candidates should fill in the PH form(https://tanzania.iom.int/vacancies), submit CV and cover letter indicating Vacancy Notice number with 3 professional references and contacts to tzvacancy@iom.int

Or send applications to the address below;

International Organization for Migration Mission in the United Republic of Tanzania
Slipway Road, off Chole Road, Plot # 1365 Msasani. PO Box 9270 Dar es Salaam, Tanzania

Kindly note only shortlisted candidates will be contacted.
For further information, please refer to: https://tanzania.iom.int 
============

DRIVER (3 POSTS) 

POSITION DESCRIPTION:

Under the general guidance of the Head of Sub Office and the direct supervision of Resource Management Officer, the incumbent will be responsible for driving vehicles to transport persons and goods authorized by IOM, from one destination to another as scheduled in safe and cost effective manner. 

APPLICATION INSTRUCTIONS:

Interested candidates should fill in the PH form(https://tanzania.iom.int/vacancies), submit CV and cover letter indicating Vacancy Notice number with 3 professional references and contacts to tzvacancy@iom.int

Or send applications to the address below;

International Organization for Migration Mission in the United Republic of Tanzania
Slipway Road, off Chole Road, Plot # 1365 Msasani. PO Box 9270 Dar es Salaam, Tanzania

Kindly note only shortlisted candidates will be contacted.
For further information, please refer to: https://tanzania.iom.int/ 
==========





Tuesday, 15 March 2016

KATIBU MKUU NACTE AJIUZULU

Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Elimu ya Vyuo vya Ufundi (NACTE), Dk. Primus Nkwera amejiuzulu nafasi yake.

Uamuzi wa kujiuzulu kwa Dk. Nkwera ulitangazwa katika ofisi kuu za Baraza hilo zilizopo Mikocheni Dar es Salaam juzi na Mwenyekiti wa Bodi,Mhandisi Steven Mlote na kusababisha baadhi ya wafanyakazi kuangua kilio.

Akizungumza katika kikao cha dharura cha wafanyakazi wote wa baraza hilo, Mlote alisema Dk. Nkwera amejiuzulu ili kulinda hadhi ya Nacte kutokana na habari iliyoandikwa na Gazeti la Dira ikimtuhumu mambo mbalimbali.

Gazeti hilo la Dira la Jumatatu tarehe 07/03/2016 toleo no.405 lilimtuhumu Katibu Mtendaji wa NACTE, Dk. Primus Nkwera kughushi vyeti vya shahada ya uzamivu baada ya kusomeshwa na serikali Afrika Kusini na kufeli.

Mlote alisema kwa mujibu wa Dk. Nkwera, nafasi hiyo haipaswi kushikwa na mtu mwenye tuhuma ya aina yoyote, na ametafakari na kuona ajiweke kando na uongozi wa Nacte ili uchunguzi ufanyike akiwa pembeni.

"Tumetumia muda mwingi kutafakari hoja ya Dk. Nkwera na hatimaye tumekubali kujiuzulu kwake kwa shingo upande," alisema Mlote na kuongeza:

"Kazi kubwa iliyofanywa na Dk. Nkwera akiwa kiongozi wa Nacte inafahamika na kila mmoja, vilio na machozi ya wafanyakazi wenzake yanadhihirisha kuwa kujiuzulu kwake kunaacha simanzi kubwa.

"Najua mmepata mshtuko mkubwa, lakini Dk. Nkwera hajafa, yuko hai na huyu bado ni mtumishi wa serikali. Alichofanya ni kuamua kuachana na ukatibu utendaji.

"Tutaendelea kumtumia itakapobidi kwa ushauri.Wakati mwingine lazima mkubaliane na hali hii, lakini pia endeleen kuchapakazi kwa ufanisi kama kawaida kana kwamba bado mko na Dk. Nkwera."

Kutokana na kujiuzulu kwake, Mlote alisema bodi imemteua Mkurugenzi wa Mitaala wa Nacte, Dk Adolf Rutayunga kukaimu nafasi hiyo wakati taratibu nyingine zikiendelea.

Aliyekuwa Katibu Mtendaji wa NACTE, Primus D Nkwera (kulia) akifafanua jambo

RAIS MAGUFULI AWA MBOGO,ASEMA KIJANA ASIYETAKA KUFANYA KAZI ALAZIMISHWE AKIKATAA APELEKWE KAMBINI KINGUVU,SOMA HAPO KUJU

Rais John Magufuli leo amewaapisha wakuu wa mikoa wapya aliowateua hivi karibuni na katika hotuba yake amewataka wakuu wa mikoa hao wapya kuhakikisha vijana wanafanya kazi na kuacha uzembe.

Rais Magufuli amewataka wakuu wa mikoa hao kuhakikisha hakuna vijana ambao watakuwa wanakwenda kucheza pool table asubuhi na badala yake vijana hao wanatakiwa kufanya kazi kweli kweli hata kwa kulazimishwa.


"Nimeamua kuwateua wakuu wa mikoa nikiamini kwamba mtaniwakilisha vizuri katika mikoa yenu.

"Napenda niwape pole kwa sababu mtakwenda kufanya kazi kweli kweli kutatua kero za wananchi wetu.

"Lakini pia niwaombe wakuu wa mikoa mkasimamie watu wafanye kazi hasa vijana.

"Haiwezekani vijana leo hii unawakuta saa mbili asubuhi wanacheza Pool table wakati wakina mama wanalima shambani, kama hawataki kufanya kazi kwa kupenda walazimishwe kufanya kazi. Atakayekataa mpelekeni kambini akafanye kazi" amesema Rais Magufuli


Rais Magufuli ameongelea pia suala la wafanyakazi hewa kwenye Halmashauri zote nchini ambapo amewapa siku 15 wakuu wapya wa mikoa kuhakikisha hakuna wafanyakazi hewa katika Halmashauri zote nchini.

"Niwape grace time ndani ya siku 15 wakurugenzi wawe wamejumlisha na wamewatoa wafanyakazi hewa katika payroll



"Mshahara wa mwezi tukigundua mkurugenzi amelipa mshahara hewa ajue hana kazi na tunampeleka mahakamani
"Singida na Dodoma ina wafanyakazi hewa 202 wanalipwa mishahara hewa na kwenye data ilionyesha wengine wamefariki, wamestaafu, wamefukuzwa , wengine likizo bila malipo wote hao kumbe wanalipwa malipo ya serikali fedha ambazo zingetumika kutatua matatizo ya wananchi" 

"Nimeamua kuwateua nyinyi kama wakuu wa mikoa nikiamini mtaniwakilisha vizuri popote.

"Nyinyi mna mamlaka ya kuwaweka watu ndani( selo) hata masaa 48,wekeni watu ndani ili wajue mnatakiwa kuheshimiwa.



"Tusiogope kuchukua maamuzi, nafuu uchukue maamuzi hata kama ni mabaya yatarekebika huko mbele."Amesema Rais Magufuli.


ZANZIBAR KUNAWAKA MOTO, MABOMU YANALIPULIWA HOVYO



Watu wasiojulikana wamerusha bomu katika nyumba ya kamishina wa Polisi Hamdani Omar Makame katika eneo la Kijichi huko zanzibar.

Nyumba kadhaa ikiwemo ya Kamishna Polisi Zanzibar H. Makame zaharibiwa baada ya kutokea mlipuko, Polisi yasema leo. Watu 31 mbaroni (Chanzo: ITV)

UPDATES:
Pemba hali ni tete, vurugu kati ya maafsaa wa polisi na raia zimeripotiwa hii Leo huku mamia ya wapemba wakikimbilia Mombasa katika nchi jirani ya Kenya.

Ikumbukwe vurugu hizi zinakuja ikiwa ni Siku moja tu baada ya Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi visiwani humo ndugu Jecha kutoa waraka wake kwa vyombo vya habari kuwa hali ya usalama visiwani humo ni salama na Amani.





Ni kweli Rais Magufuli kawapunguzia Ulinzi wastaafu Jakaya Kikwete na Mkapa? ninayo hii kutoka IKULU



Kwenye Gazeti la JamboLEO, toleo namba 2381 la tarehe 15 March 2016 limechapisha taarifa yenye kichwa cha habari kisemacho “Magufuli awapunguzia ulinzi marais wastaafu”

Taarifa yake kamili ipo katika ukurasa wa nne na inaeleza kuwa Rais Magufuli amewapunguzia ulinzi Marais wastaafu na imewataja marais hao kuwa ni Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete.

Ikulu inapenda kuwataarifu watanzania kuwa taarifa hizo sio za kweli na inalitaka gazeti hilo kukanusha habari hiyo mara moja, vinginevyo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Taarifa iliyotolewa kupitia kwa kaimu mkurugenzi wa mawasiliano, IKULU Gerson Msigwa ni kwamba pia IKULU inasisitiza kwamba Watanzania wanatakiwa kufahamu kuwa utaratibu wa ulinzi wa Marais wastaafu haujabadilishwa


UCHAGUZI WA MEYA WA JIJI LA DAR NI TAREHE 22 MARCH

Uchaguzi wa meya wa jiji la dar es salaam umepangwa kufanyika 22.03.2016 siku ya jumanne (siku ya kazi )katika ukumbi wa Karimjee kuanzia saa 4.00 asubuhi. Katika barua za mwaliko wabunge, madiwani na viongozi wa chama.,Kaimu Mkurugenzi wa jiji la dar amepiga marufuku watu wasiokuwa na mwaliko kufika ukumbini Karimjee kushuhudia hilo zoezi la uchaguzi.

Man Gets Stuck To Another Man’s Wife After S€x







A Twitter user, @Kevin_teya, is claiming that a guy in Kitale, Kenya had S€x with someone’s wife and he got stuck. The man and the woman glued together after they enjoyed themselves in hotel. It was alleged that the husband of the promiscuous woman set up the concubine with spiritual voodoo.

NAIBU WAZIRI WA AFYA ALIFOJI VYETI: BASHE ANASEMA


Sikuwahi kuwa member wa hii forum
lakini nimeguswa na kuvutiwa kutokana
na mjadala ambao umemhusisha Mbunge
wangu MH HAMIS ANDREA KIGWANGALA
(SAIDI NASSOR BAGAILE) sikutaka
kujadili jambo lolote lakini
kilichonileta hapa kuchangia ni
mambo makubwa mawili ambayo
nitayataja hapa chini, leo
nimefahamu kwanini Mh Kigwangala
tulipokutana mara ya mwisho pale
MOVENPICK Ijumaa katika kujadili
baadhi ya mambo na umuhimu wa social
network nikamwambia nataka nijiunge
na wana bidii, alinishauri
NISIJIUNGE WANABIDII KWAKUWA NI
SEHEMU ISYOFAA WATU WANAPINGA KILA
KITU, nimefahamu sababu kumbe
hakutaka nifahamu kuwa mbunge wagu
yupo huku akipotosha taarifa nyingi
sana. Sikupenda kujibu hoja zake
imenibidi,hizi chini ni sababu kuu
zilizonisukuma kujibu.
(1) Mbunge wangu amenitaja kwa jina
katika baadhi ya mambo.
(2) Kuweka rikodi sawa sawa juu ya
baadhi maswala ya Msingi.
Hizo ni sababu kubwa zilizonifanya
niingie na kujibu baadhi ya
mambo,nimesoma hoja za Mbunge
ameongelea maeneo makuu yafuatayo,
(1) UHALALI WA JINA LAKE (2) URAIA
WA BASHE (MIMI BINAFSI) (3) AMESEMA
HAKUBEBWA ( 4) AMONGELEA USHINDI
WANGU (5) AMEONGELEA SWALA LA WAMA
( 6) AMEONGELEA KUWA ALIRUDISHA
UNITY KTK CHAMA (7) ASILI YAKE. Haya
ni maeneo makuu niliyoweza kuyaona
katika majibu yake alotoa hapa.
Nianze kwa kusema HAKUNA JAMBO BORA
DUNIANI KAMA KUFAHAMU MAPUNGUFU
YAKO, KUYAKUBALI NA KUKUBALI
KUYAFANYIA KAZI, PIA HAKUNA JAMBO
BORA KAMA KUMSHUKURU MUNGU KWA JAMBO
LOLOTE UNALOKUTANA NALO kama
nilivoshukuru mimi tar 2 august 2010
baada ya kuapata ushindi wa kura za
maoni, na kushukuru pia baada ya
kutoteuliwa na chama vyote
nilimshukuru mungu.
Nimesema haya maneno kutokana na
mbunge wangu kutokuwa mtu
wakushsukuru mungu kwa bahati
alopata ambayo imetokana na tabia na
mila za watu kumalizana kutokana na
kuwa na misimamo,mitazamo,fikra,na
maoni tofauti tofauti juu ya baadhi
ya mambo.SAIDI be a Gentleman kubali
ubunge wa jimbo la Nzega haukuwa
wako hukuwa na political Vission,
Mission, wala strategy ya kupata
ubunge ule,bcs of CCM politics Mimi
na Lucas selelii hatukuteuliwa and
you KNOW it.
NIANZE NA UHALALI WA JINA:
Usipotoshe watu jina la Hamis Andrea
si jina lako kijana mwenye jina hili
yupo Nzega unafahamu na baada ya
Wewe KUTEULIWA Chama na Wana CCM
kilikushauri uende mahakamani kuapa
kupata kiapo cha mahakama kubadili
jina na kulichukua rasmi jina la
Hamis Andrea na ulifanya hivo, jina
la hamis andrea umelichukua Rasmi
baada ya KUTEULIWA na kabla ya
kuchukwa Form na kuhisi utawekewa
Pingamizi, lakini deep in your heart
uanafahamu wewe na mimi tumesoma same
primary school na mimi na wewe
hatukufaulu DARASA LA SABA KITONGO
PRIMARY SCHOOL.
Baada ya hapo kutumia nafasi ya mama
yako ambae wakati huo alikua ni
mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Nzega
ulienda mwanzoli ukachukua jina la
HAMIS ANDREA na kuanza kulitumia
kijana huyu alifaulu yeye na watoto
wa MZEE MTANGA WAKIKE AMBAO NI TWINS
kwakuwa hakuwa na taarifa mapema na
kwa kuwa kijana huyu baada ya
kumaliza pale mwanzoli alienda kuishi
KITANGILI baada ya mitihani taarifa
za ufaulu wake zilichelewa kumfikia
kijana huyu, ulichukua nafasi yake
na wewe kwenda KIGOMA SEKONDARI.
Ni kweli kama ulivosema kwamba wewe
nimjukuu wa mzee KIGWANGALLAH,huu ni
ukoo wa mama yako na si BABA yako,na
tulipokuwa tunasoma Primary ulikuwa
unaitwa Jina la SAIDI NASSORO
BAGAILE, nayo haya majina ( nassoro
bagaile) ni ya ukoo wa mama yako
tumekuwa wote hatumjui BABA YAKO na
hakuna mtu wa Nzega ambae anamfahamu
baba yako na siku zote imekuwa HIVYO
until utakapo prove otherwise
( tunaweza kuchanga fedha hapa
wanabidii watafute team ya watu
wakafanye uchunguzi walete ripoti
hapa tujue nani mkweli). Wanabidii
mkiangalia HOJA ya kuhalalisha na U
TANZANIA WA KIGWANGALA SIKU ZOTE
ATAELEZA KWA KIREFU HISTORIA YA
UPANDE WA MAMA YAKE UPANDE WA BABA
UTABAKI UNCLEAR HATA MAELEZO YAKE
HAPA YANAONYESHA HIVO,ingawa haikuwa
strategy yangu kum disqualify SAIDI
baada ya kuteuliwa katika uchaguzi
kwa HOJA YA UIRAI bcs mimi si
MUUMINI WA UKABURU HUO. USHINDI WANGU 2010
Mh Saidi/kigwangala amekuwa mara
nyingi akitaka kupotosha ukweli juu
ya ushindi wangu labda watu wengi
wajue historia ya mimi na wewe
katika siasa za JIMBO LA NZEGA,2005
wote tukiwa tumetoka mashuleni na
ajira zetu za mwanzo tuligombea
ubunge jimbo la nzega wewe ukitumia
Gari aina ya Mark 11 na mimi Suzuki
vitara ukiwa na mkeo mimi single
ukipita kuwaambia wananzega
wakuchague kwakuwa wewe ni msomi,
kijana na una mke.
Huku mimi nikipita na kuwaambia
wanichague kwa kuwa mimi ni kijana
wao wamenisomesha na sasa nina taka
kusimamia yale ambayo waliotangulia
walishindwa kuyafanya.
Wana CCM wajimbo la Nzega walinipa
kura 109 na wewe kura 24 chini ya
25% ndicho ulichopata ukifananisha
ushindi wangu na wako, wakati huo
kaka yetu LUCAS SELELII akipata
ushindi wakura zaidi ya 300.
Baada ya hapo wewe ulikimbia jimbo
hukushiriki jambo lolote wakati mimi
nikiendelea kutekeleza yake
niliyoahidi kwa wapiga kura kama
ninavyofanya sasa, 2007 ulifanyika
uchaguzi wa chama nikapa kura 1947
kati ya kura 1982 zilizopigwa na
mimi kuchaguliwa mjumbe wa mkutano
mkuu wa CCM TAIFA.
Then katika mktano mkuu wa mkao wa
Tabora nilipata kura 487 kati ya
kura 550 zilizopigwa na kuchaguliwa
Mjumbe wa Halmshauri kuu ya CCM mkoa
wa Tabora, chaguzi hiz wewe
hukishiriki nilishinda huku
nikipingwa na watu wote wenye Nguvu
katika MKOA namaanisha WOTE. Na hapa
nilizuia wizi wkura na GAZETI LA
MWANANCHI LILIANDIKA STORY CCM
WAONYESHA NAMNA YA KUIBA KURA.
2010 KATIKA UCHAGUZI
Katika uchaguzi huu nilishinda
kihalali katika vitua 152 wewe
uliongoza vituo 3,ambavyo nata
CENTRE ulinizidi kura 7,isanzu
centre,na shila,wakati kaka yetu
SELELII alishinda vituo Viwili
ambavyo ni SILIMUKA akinizidi kura
52,na ITILO akinizidi kura 17 kama
sikosei.
LAKINI VITUO HIVO SI KATA KIKATA
MIMI NILISHINDA KATA ZOTE 21, na
wewe unalifahamu hili tulikua na
Vituo 152 katika kata 21,vituo vyote
tuliweka mawakala wote sisi wagombea
wakuu 3 katika uchaguzi huo na
matokea yakawa Bashe 14,420,SELELII
2500 KIGWANGALA(SAIDI)1530 kama
sijakosea ukitazama kura hizo ni
sawa ni 11 to 12% ya kra nilizopata.
Wana Bidii hata leo tukirudia
Uchaguzi JIMBO LA NZEGA NITASHINDA
KWA KURA NYINGI SANA na ikiwezekana
tuakaandikishane tukafanye kampeni
nauhakika nitamshinda lakini UBUNGE
aendelee nao hili sina shaka juu
yake.
Utakumbuka wakati wa kura za maoni
niliwaahidi kuwashinda kwakuwa
nilikuwa nafahamu kuna njama hizi
nilikuambia wewe na wengine
,ninafahamu mpango wa kunikata jina
lakini nitahakikisha ninawashinda kwa
kura nyingi sana ili
hatamtakaponikata watanzania na
wananzega watapiga kelele kwa niaba
yangu na historia itakuwa imeandikwa
na hili lilitokea.
Wapo wanahabari waliokuwa wananieleza
juu ya mipango hii mliokuwa
mnaifanya na ilifahamika mapema ,but
I said to my self sijajiunga CCM kwa
ajili ya UBUNGE tu nitagombea
nitashindwa nitakatwa lakini nitabaki
ndani ya CCM kutimiza wajibu
wangu,na unafahamu hili kwa 2015 u
will face me again if god
wish,politically u have never been
threat to me jimbo la nzega
ninafahamu mtu pekee ambae ninaamini
ni threat kwangu ni LUCAS LUMAMBO
SELELII not you.
HOJA YA WAMA
Sipendi kuliongelea sana hili lakini
ni AJABU unapokana kuwa HUKUWAHI
KUFANYA KAZI NA WAMA ni kama mimi
nije katika PUBLIC nisema siajawahi
kuajiriwa na ROSTAM AZIZ ni kukana
ukweli ulio wazi binafsi sina
uhakika kama uteuzi wako una
mahusiano na kazi zako WAMA.
Bali nina uhakika umefanya kazi za
WAMA kama MUWEZESHAJI na MTOA
mafunzo yapo maeneo ambayo
uliwahikutoa TRAINING ambayo mimi
nafahamu,mfano KANDA YA ZIWA umewahi
kufanya maeneo kama shinynga ,BARAZA
KUU LA UVCCM ambalo mimi nilikuwepo
DODOMA 2008 feb uliletwa na WAMA why
useme UONGO jambo baya sana
najisikia AIBU MBUNGE WANGU ANAPO
DANGANYA.inawezekana mpaka leo
tunasubiri maandamano ya kufunga
mgodi hakuna umetudanganya naanza
kupata mashaka na wewe.
USHINDI WA JIMBO LA NZEGA
Be honest huweza kufanya mkutano wa
HADHARA hata mmoja mpaka ALIPOKUJA
MH RAIS na sote tuliahidi
kukusaidia,mimi ni mmoja wa watu
ambao waligombana na MARAFIKI zangu
kuja kukuombea KURA ni utamaduni
mwema mtu kushukuru unafahumu deep
inside in ur heart hukuwa na team ya
kampeni aliekuwa kampeni meneja wako
MR RWANGISA ndie aliekuwa kampeni
MENEJA WA KAKA YETU SELELII,leo
unasema HUKUBEBWA ULIBEBWA NA CCM na
wana nzega walichagua chama
kilichotuokoa NZEGA kama chama ni
UPINZANI kugawanyika CUF na CHADEMA
ur un popular katika JIMBO NA HILI
UNALIFAHAMU.
UNITY KATIKA CHAMA
SAIDI/KIGWANGALA wana ccm waliungana
kukisaidia chama chetu nah ii
haikuwa jitihada yako binafsi wala
jitihada ya mtu mwingine wewe si
ulieleta umoja katika chama bali
itikadi z wana ccm ndizo zilizo
waunganisha watu wa nzega na
ukiangalia katika historia yetu ya
jimbo this time ni mwaka ambao watu
walijitokeza kidogo kuliko
waliojiandikisha,hukupata hata kura
za wanachama wa ccm walipiga kura
wote,utakumbuka binafsi nilipita
maeneo yote ambayo wewe ulishindwa
kuyafikia ulienda maeneo hayo baada
ya mimi kuwa nimepita na kueleza why
wachague CCM na sikuwahi kutumia
JINA lako kuombea kura chama BCS
nilijua the only instrument ya
kuwafanya wana Nzega wakuchague ni
kutumia CCM.
HITIMISHO
Wana bidii mara nyingi MH mbunge
wangu amekuwa akitaka tuamini kwamba
yeye A kumbe ni B its good kusimama
kwa RANGI yako sikupanga kuyaongea
haya lakini imenilazimu kufanya hivo
baada ya kuwa mara zote nikiangalia
mkuu wangu akipotosha ukweli juu ya
mambo mengi.
Jambo la msingi kubali hukushinda
nzega ,hukuwa chaguo la wana
nzega,umefaidika na migogoro ya
kisiasa ndani ya mkoa na Taifa
hili,leo usilazimishe watu wakaanza
kufanya kazi kuangalia CREDIBILLITY
ya hata ELIMU YAKO NI QUESTIONABLE,
ukiangalia unaongela umesoma MASTERS
ya Bsness Administration, KAROLINSKA
institute a lot of questions with no
answer.
Tutaangalia credibility ya Degree
yako ya Muhimbili,tutaangalia
uhalali wa wewe kuchukua kiapo cha
kubadili jina siku tatu kabla ya
kujaza fomu,usilazimishe tujadili
ambayo si sawa kuyajadili wewe ni
kiongozi sasa acha siasa za
uongo,upotoshaji,simamia
unachokiamini na si wanachokiamini
wengine.
Tutahoji moral authority juu ya
mambo mengi unayoongea wakati wewe
ni mmoja wa walio benefit na
STIMULUS package 2009/10 ambazo
hazikuwafaidisha wakulima zaidi ya
kujinufaisha wewe binafsi kununua ma
Range mjini na kuja kugombea ubunge
Nzega kwa Fedha za walipa Kodi
kupitia kampuni ya MSK ambayo
wananchi wa Nzega hiuta jina la
Ambalo unalifahamu,,tutakuhoji
uadilifu wako wakati wewe ni mtu
alilazimisha wananchi wa nzega waache
kulima mazao ya chakula walime PAMBA
kujinufaisha wewe binafsi na biashara
yako na kushindwa kuwapa pembejeo
matokea yake PAMBA wakose na chakula
wakose.
Na sasa wanakabiliwa na njaa ukitumia
nafasi yako ya ubunge kuhamasisha
kilimo cha pamba na matokeo yake
kuwatia watu umasikini na sasa wana
nzega wanakabiliwa na njaa,
Umefika wakati wa wewe kusimamia
ahadi ulizotupa jimboni Tunasubiri
maandamano siku 21 zimeisha,na hapa
nilikushangaa lakini nikakubali
kujifunza kitu kipya Mgodi ule upo
pale kisheria,ni ilani ya chama
uliyoinadi,leo unaandaa maandamano
kuondoa?
Nikasema labda new approach ktk
siasa zetu,Umetuahuahidi mikopo kina
mama nzega umechukua viingilio vyetu
hujatoa mkopo mpaka leo ni either
urudishe 6000 ulizochukua ama uwape
mikopo,sio kupita na kuchinja
Ng”ombe na pilau vijijini ndio
maendeleo tuliotaka wana nzega.
Sikutaka kujakutoa maelezo marefu
hapa,kama nilivokushauri juzi wakati
tunachangia mfuko wa maendeleo wa
mkoa wa TABORA Yule kijana unajua
unatumia jina lake unajisikiaje
anabeba mizigo sokoni na
GANAGANA,msaidie mtafutie mtaji
akafanye biashara hata nje ya Nzega
kwa Mungu utaoneka umeshukuru,bila
ya Jina lake leo may be usingekuwa
hapo ulipo una RESPONSIBILITY YA
KIBINAADAMU KUMSAIDIA YULE BWANA
HAMIS.
Mwisho kuwa mkweli ukweli utakuweka
HURU

Featured post

MWANAMKE YAFUATE HAYA; NI MUHIMU KWA MAHUSIANO YAKO

1. Degree yako ya fist class uliyoipata chuo kikuu haiwezi kukufanya uwe mke first class katika ndoa yako bali ni heshima yako na uthubu...