Kuna wakati fulani niliamua kwenda dukani pale mijini Dodoma katika duka la mfanyabiashara mmoja maarufu sana.Lengo la kwenda pale
lilikuwa kununua nguo(suti).Sasa mimi niliamua kununua suti manake kulikuwa na
sherehe maalumu sana nilikuwa nimealikwa na mmoja wa rafiki zangu nyumbani kwa
mbunge mmoja pale area D.Mimi kwa kuwa nilijua suruali navaa kiuno namba
fulani,basi sikuhangaika kujipima ile suti.Iliangaliwa tu kwa nje na baada ya
kuona namba ya suruali basi nikanunua.Kwa bahati mbaya mimi huwa napenda
nikinunua vitu nipewe na risiti.Nilipewa risiti na kuondoka dukani.Kufika
chuoni sikujaribu ile suti hadi siku ya jumamosi nilipomaliza kuoga ndio
nikafungua mfuko na kuvaa suti.Cha kushangaza suti ile ilikuwa kubwa sana
kwangu.Suruali ilikuwa imezidi inchi tano kiunoni na pia ilikuwa ndefu sana.Pia
lile koti la suti lilikuwa pana kuliko mimi na mikono yake ni mirefu kiasi cha
kufunika kabisa mikono yangu.Nisingeweza kuirudisha dukani kwa kuwa risiti
iliandikwa maneno “Goods once sold are not returned).kwa maana hiyo nilijifunza
kuwa sitanunua tena nguo yoyote bila kuijaribisha kama inanikaa na kama nikivaa
napendeza.Labda nianze kwa kukuuliza ndugu msomaji wangu,je? Wewe unaweza
kununua nguo bila kuijaribu?Naamini jibu litakuwa ni hapana.Lazima uijaribu
kwanza.
Watu wengi hupenda hutumia mfano huo kuhusu ndoa.
Wanaona ni afadhali mwanamume na mwanamke kuishi pamoja kabla ya kuoana
kisheria. Wao wanasema ‘mambo yakienda mrama, wanaweza kutengana bila
kukabiliana na matatizo ya talaka kwa kuwa eti Masuala ya talaka yanayogharimu
sana.
Inawezekana baadhi ya wale walio na maoni kama hayo
wamemwona rafiki yao aliyefunga ndoa akivumilia ndoa mbaya. Au huenda wengine
wakawa wamejionea hali mbaya za ndoa ambayo mume na mke hawapendani tena. Kwa
sababu hiyo, huenda wakaona kuishi pamoja bila kufunga ndoa kuwa jambo lenye
hekima ili kuzuia matatizo ya baadaye,au wakaamua kuishi pamoja kwanza ili
kusomana tabia zao.
Biblia ina maoni gani kuhusu jambo hilo? Ili kupata majibu sahaihi, tunahitaji kuchunguza kile
ambacho Neno la Mungu linasema kuhusu ndoa.
“Mwili Mmoja”
Biblia
inaheshimu sana ndoa, na hilo halishangazi kwa kuwa mpango wa ndoa
uliidhinishwa na kuanzishwa na Mungu
mwenyewe. (Mwanzo 2:21-24) Tangu kuumbwa ulimwengu, Mungu alikusudia kwamba
ndoa iwaunganishe mwanamume na mwanamke kuwa “mwili mmoja.” (Mwanzo 2:24) Baada ya kunukuu maandiko matakatifu ya Biblia kuhusu jambo
hili, Yesu aliongezea hivi: “Kile ambacho
Mungu ameunganisha mtu yeyote asikitenganishe.”—Mathayo 19:6.
Ni
kweli kwamba wengine ambao hufunga ndoa baadaye hupeana talaka(Baada ya kuishi
pamoja muda mrefu). Watu
hawatalikiani kwa sababu kuna tatizo na mpango wenyewe wa ndoa; badala yake
wanatalikiana kwa sababu mwenzi mmoja au wote wawili walishindwa kuheshimu
kiapo walichotoa siku ya arusi yao.
Kwa mfano: Tuseme mwanamume na mwanamke wana gari,
lakini hawalitumii kulingana na maagizo yaliyotolewa na mtengenezaji wake. Nani
atalaumiwa gari hilo linapoharibika? Je, ni mtengenezaji au ni wenye gari ambao
walishindwa kulitumia kutokana na maelekezo ya mtengenezaji?
Kanuni hiyohiyo inahusu ndoa. Mume na mke
wanapodumisha uhusiano wao na wanajitahidi kutatua
matatizo yao kwa kutumia kanuni za Biblia, si rahisi watalikiane. Wanajihisi
wakiwa salama katika ndoa ile kwa kuwa kila mmoja anawajibika kwa mwenzake. Kwa
sababu hiyo ndoa inakuwa msingi wa uhusiano wenye upendo.Na inafikia hata hatua
ya kuwa na damu za aina moja.Jiulize kwanini watu wakioana na wakaishi kwa
upendo ukiwatazama sura zao ni kama zinafanana?
“Mjiepushe na Uasherati”
Lakini bado huenda wengine wakajiuliza: ‘Kwa nini basi
tusiishi pamoja kwanza? Je, kujaribu uhusiano huo kabla ya kuanza kuwajibika si
kunaonyesha kwamba tunaiona ndoa kuwa takatifu?’
Biblia
inatoa jibu la wazi. Paulo aliandika: “Mjiepushe na uasherati.” (1 Wathesalonike 4:3) Neno “uasherati” linamaanisha mahusiano yote ya ngono
nje ya ndoa. Hilo linahusisha ngono kati ya watu wawili wanaoishi pamoja, hata
kama wanakusudia kuoana. Kulingana na maandiko matakatifu, basi ni kosa kwa
watu wawili kuishi pamoja kama mume na mke hata ikiwa nia yao ni kuoana
baadaye.
Kwa bahati mbaya vijana wengi kutokana na maendeleo ya
sayansi na teknolojia yaliyopelekea kubadilika mfumo wa maisha wanadhani
maadiko hayo yamepitwa na wakati. Isitoshe, katika nchi nyingi, ni jambo la
kawaida kwa watu kuishi pamoja—iwe wanakusudia kuoana au la, na mahali pengine
watu wanaishi kwa mkataba kabisa. Lakini fikiria matokeo ake ni yepi hasa?. Je,
wale wanaoishi pamoja wamepata mafanikio katika familia hiyo? Je, wana furaha
kuliko wale waliofunga ndoa? Je, tarakimu zinaonyesha kwamba wenzi wa ndoa
walioishi pamoja kabla ya kuoana ni waaminifu kuliko wale wengine? Uchunguzi
unaonyesha matokeo tofauti kabisa. Kwa kweli, imeonekana kwamba wenzi wa ndoa
walioishi pamoja kabla ya kufunga ndoa wana matatizo mengi zaidi ya ndoa na
mwishowe hutalikiana.Maana yake ni kwamba hakuna uhusiano wa karibu na ulio wa
afya kati ya kuishi pamoja kabla ya ndoa na mafanikio baada ya kufunga ndoa
hiyo.
Wataalamu toka Ireland wanasema kwamba uchunguzi kama
huo una kasoro. “Watu wanaoamua kufunga ndoa bila [kuishi pamoja] kwanza wana
mtazamo tofauti kabisa na watu wanaoamua [kuishi pamoja] kwanza,” anaandika
mtaalamu mmoja wa saikolojia. Anasema kwamba jambo kuu si kuishi pamoja; badala
yake jambo kuu ni “kuthamini ile hali ya kuoana.”
Hata
ikiwa hilo ni kweli, linakazia tu umuhimu wa kusitawisha maoni ya Mungu kuhusu
ndoa. Biblia inasema: “Ndoa na iheshimiwe na watu wote.” (Waebrania 13:4) Mwanamume
na mwanamke wanapoapa kuwa mwili mmoja
na kuheshimu mpango wa ndoa, wanakuwa na kifungo kisichoweza kukatwa kwa
urahisi.—Mhubiri
4:12.
Kwa
hiyo, tukirudi katika mfano wa kwanza, ni jambo
linaloingia akilini kujaribu suti au vazi kabla ya kulinunua. Hata hivyo, wazo
hilo haliungi mkono kuishi pamoja kabla ya ndoa. Badala yake, mtu anapaswa
kutumia muda kumfahamu yule anayekusudia kumuoa au kuolewa naye. Hiyo ni hatua
muhimu ambayo mara nyingi hupuuzwa lakini ni moja kati ya siri za
kufanikiwa kwa familia na kuwa na ndoa yenye amani na furaha wakati wote.
Biblia imeweka mkazo na kusisitiza tendo la ndoa kati
ya waliooana tu-Zaburi 84:11;1 Wakorintho 6:18.Kwa hiyo wanaoishi pamoja kabla ya kuoana/ndoa
wanavunja amri hii ya Mungu na wanamchukiza ungu kwa kuwa wanalala na kufanya
ngono kama mume na mke kabla ya kuwa na agano halaliyaani ndoa.
Kuishi
pamoja kabla ya kufunga ndoa hakutoi nafasi ya nyie kusomana…la hasha.Pale
mnaisho tayari kama mme na mke japo kwa wizi.Biblia imeainisha njia bora na
vigezo vya wazi vya namna ya kumsoma mwenza wako wa maisha mkiwa hamuishi
pamoja-Rejea…..Ruthu 1:16, 17; Methali 31:10-31. Biblia inasema: “Yeye aliye na mazoea ya kufanya
uasherati anautendea dhambi mwili wake mwenyewe.” (1 Wakorintho 6:18) Katika miaka ya karibuni, ukweli wa maneno hayo
umeonekana kwa sababu ya mamilioni ya watu ambao wamekufa kutokana na UKIMWI na
magonjwa mengine ya zinaa. Lakini si hilo tu. Uchunguzi umeonyesha kwamba ni
jambo la kawaida kwa vijana wanaofanya ngono kushuka moyo sana na hata kujaribu
kujiua. Pia, ukosefu wa maadili husababisha mimba zisizotakiwa, na hilo
hutokeza katika visa fulani kishawishi cha kutoa mimba. Kwa kufikiria mambo
hakika, tunaweza kukata kauli kwamba sheria ya maadili iliyo katika Biblia haijapitwa na
wakati.
Hujachelewa,Mlango bado iko wazi kutubu na kujisahihisha.
Endelea kunifuatilia kupitia bLOG hii ujipatie maarifa zaidi
Karibu sana!!
No comments:
Post a Comment