Watu wasiojulikana wamerusha bomu katika nyumba ya kamishina wa Polisi Hamdani Omar Makame katika eneo la Kijichi huko zanzibar.
Nyumba kadhaa ikiwemo ya Kamishna Polisi Zanzibar H. Makame zaharibiwa baada ya kutokea mlipuko, Polisi yasema leo. Watu 31 mbaroni (Chanzo: ITV)
UPDATES:
Pemba hali ni tete, vurugu kati ya maafsaa wa polisi na raia zimeripotiwa hii Leo huku mamia ya wapemba wakikimbilia Mombasa katika nchi jirani ya Kenya.
Ikumbukwe vurugu hizi zinakuja ikiwa ni Siku moja tu baada ya Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi visiwani humo ndugu Jecha kutoa waraka wake kwa vyombo vya habari kuwa hali ya usalama visiwani humo ni salama na Amani.



No comments:
Post a Comment