Saturday, 12 March 2016

GAVANA AMJIA JUU RAIS MAGUFULI: AKIUKA AGIZO LAKE

Hatimaye gavana wa BoT Prof. Beno Ndulu ametoa majibu kwa rais John Magufuli huku akisisitiza kuwa watu wanaongea wasiyoyajua na kuomba apewe majina pamoja na taarifa za wale watu wanaodhani kuwa ni wafanyakazi wasio na umuhimu BoT.

Hayo yanajiri siku moja baada ya rais John Magufuli kumuagiza gavana huyo kuwaondoa ndani ya utumishi wa BoT wafanyakazi wote wasio na umuhimu pamoja na wale wanaojulikana kuwa ni wafanyakazi hewa.

Jana gavana akiongea na vyombo vya habari pamoja na gazeti la MTANZANIA alisema kuwa kila mfanyakazi wa BoT ana umuhimu wake huku akisisitiza kuwa watu wanaongea wasiyoyajua. Prof. Ndulu pia alisisitiza kuwa yule anayedhani kuwa kuna wafanyakazi wasio na umuhimu BoT basi ampelekee majina yao pamoja na taarifa zao!

Hata hivyo gavana huyo aliweka wazi kuwa rais ametoa agizo hivyo ni muhimu kuzingatia agizo la rais lakini akaweka mkazo kuwa BoT itajiridhisha kwa kina kwanza kabla ya kuchukua hatua yoyote ile! 

My take: Jana nilileta thread humu huku nikisisitiza kuwa huenda rais hajui kile anachokizungumza kuhusu BoT na nikaenda mbali zaidi kuelezea namna utumishi ulivyo pale BoT! Watu mkaja na povu huku mkituma mashambulizi ya kila aina! Haya na leo mjibuni Beno Ndulu! Au mwambieni rais atumbue majipu!

BoT ni taasisi nyeti iliyobeba wafanyakazi ambao kimsingi wanawajibika kwa kina kuhusu nchi! BoT ni taasisi iliyounganishwa kimataifa!


HUYU HAPA KATIBU MKUU WA CHADEMA

Ni asubuhi tulivu ya Jumamosi hapa Jijini Mwanza.

Wananchi hapa wanasubiri ujio mkuu leo.Ujio wa Katibu mkuu wa Chama chenye ufuasi mkubwa nchini cha Chadema.

Kiongozi mkuu wa upinzani nchini Freeman Mbowe ndiye atakayesimama leo mbele ya Baraza Kuu kutegua kitendawili kinachosubiriwa kuteguliwa na mamilioni ya wafuasi ndani na nje ya nchi.

Tayari majina kadhaa yasiyopungua kumi yamekuwa yakibashiriwa kwamba moja kati ya hilo ndilo litakalopita katikati ya moshi mweupe pale kwenye ukumbi wa Gold Crest.

Hekima na busara nyingi za Freeman Mbowe zimesababisha mpaka leo jina hilo kuwa siri kuu.Hata hivyo uchunguzi wa kuaminika kutoka kwa watu wa karibu na washauri wakuu wa Freeman Mbowe unasema Katibu mkuu mpya atakuwa ni mpenda chama na wananchi,kiongozi asiyeyumbishwa,mtetezi wa Katiba ya chama na jasiri asiyeyumbishwa atakayekuwa na uwezo wa kutamka jambo na nchi inasimama.

Waandishi wa habari wa ndani na nje ya nchi wamefurika kwenye viunga vya ukumbi huu kujiandaa kuwa wa mwanzo kurusha jina la Katibu mkuu mara litakapotangazwa.

Mtandao huu wa JESAM utakuletea jina hilo mata tu litakapotajwa 

STORI YENYE KISA KIZITO: SOMA IKUFUNZE

“Nilipofika nyumbani usiku ule, mke wangu
aliponitayarishia chakula, nilimshika mkono na
kumwambia, Kuna kitu nataka nikwambie. Mke wangu
alikaa chini na kula chakula kimya akiwa tayari
kunisikiliza. Tena nikagundua macho yake yalionyesha
anaumizwa. Nilishindwa hata namna ya kuanza
kufumbua kinywa changu. Lakini ilibidi nimwambie ili
ajue nilikuwa nikifikiri nini juu yake.
Nataka kukupa talaka. Nilianza kusema kwa utulivu.
Alionekana kutokereka na maneno yangu badala yake
aliniuliza kwa sauti ya upole ‘kwa nini?’ Sikumjibu swali
lake. Kutojibu kulimfanya akasirike. Akatupa kijiko na
akanikaripia, ‘wewe si mwanamume!’ Usiku ule,
hakukuwa na maongezi kati yetu. Alikuwa akilia kwa
kwikwi. Nilifahamu kwamba alitaka kujua ni nini
kimetokea kwenye ndoa yetu. Lakini kwa hakika
nisingeweza kumpa jibu wala sababu ya kuridhisha;
alionekana si mali kitu kwangu penzi langu lilihamia
kwa Mary. Sikumpenda tena mke wangu mawazo yote
yalikuwa kwa Mary. Kwa kweli nilimdharau mke wangu!
Huku moyo wangu ukijua wazi kwamba nafanya kosa,
niliandika talaka ambayo ilionyesha kwamba yeye (mke
wangu) angepata nyumba yetu, gari na atakuwa na hisa
30% ya kampuni yetu. Aliangalia talaka ile na kuichana
vipande vipande.
Mke ambaye tumeishi nami kwa miaka 10 alionekana
mgeni machoni mwangu. Nilimuonea huruma kwa
muda, rasilimali na nguvu alizopoteza lakini sikuweza
kurudi nyuma kwa sababu Mary aliuteka moyo wangu
kisawasawa. Hatimaye mke wangu alilia kwa sauti
mbele yangu, jambo ambalo kwa hakika nilitarajia.
Kwangu mimi kilio chake kilinipa nafuu.
Wazo la kuachana na mke wangu limenisumbua kwa
majuma kadhaa na sasa limeendelea kuimarika na kuwa
jambo la hakika zaidi.
Siku iliyofuata nilikuja nyumbani kwa kuchelewa sana
nikakuta mke wangu akiandika jambo mezani.
Sikutamani hata kula chakula alichonipikia nilikwenda
moja kwa moja chumbani na usingizi ulinichukua mara
moja kwa sababu nilikuwa nimechoka baada ya kula
raha za kufa mtu na Mary
Usiku nilishtuka usingizini mke wangu alikuwa bado
akiandika. Sikujali kabisa nikajifunika vyema shuka na
kulala tena. Asubuhi yake alinikabidhi masharti ya
talaka yake: hakutaka kitu chochote kutoka kwangu
lakini alihitaji apate angalau mwezi mmoja wa
kujiandaa kabla hajaachika. Akaomba kwamba katika
kipindi hicho cha mwezi mmoja sote mimi na yeye
tujitahidi kuishi maisha ya upendo au kawaida kwa
kadiri itakavyowezekana. Sababu yake ilikuwa ndogo
lakini muhimu: mwanetu wa kiume alikuwa akikaribia
kufanya mtihani katika mwezi uliofuata kwa hiyo
hakupenda mtoto aathirike kisaikolojia kwa sababu ya
kuachana kwetu. Hili halikuwa tatizo kwangu, nilikubali
mpango wake. Lakini alikuwa na sharti la ziada,
aliniomba nikumbuke jinsi nilivyombeba siku za fungate
yetu hasa siku ya harusi yetu. Akaniomba na kunisihi
kwamba katika kipindi hicho cha mwezi mmoja niwe
nambeba kutoka kitandani kwetu mpaka mlango wa
kutokea kila asubuhi. Nilidhani anakaribia kuwa kichaa.
Ili kufanya siku zetu za mwisho zisiwe na migogoro
nilikubaliana na masharti yake ya ajabu.
Nilimsimulia Mary kuhusu masharti ya kuachana na
mke wangu. Mary alicheka sana, aliona ni ujinga. ‘Hata
akitumia ujanja wa namna gani talaka ni lazima’,
alisema Mary tena kwa dharau. Mimi na mke wangu
hatukuwahi kugusana tangu nilipomweleza dhamira ya
kumtaliki. Kwa hiyo nilipombeba kwa mara ya kwanza
sote tulinuniana. Mwanetu alifurahi sana na kupiga
makofi nyuma yetu, ‘aah baba kambeba mama
mikononi mwake’. Maneno yake yalinichoma moyoni
moja kwa moja. Kutoka chumbani kwetu hadi sebuleni,
halafu tena mpaka mlangoni, ni zaidi ya mita kumi
nimembeba mke wangu. Alifumba macho na kusema
kwa sauti laini na ya upole; usimwambie mwanetu juu
ya talaka. Nilikubali kwa kichwa, ingawa nilijisikia
vibaya. Nilimuweka chini nje ya nyumba.
Alienda kituoni kusubiri basi la kazini kwake nami
nikaendesha gari kwenda ofisini kwangu. Siku ya pili,
zoezi lilikuwa rahisi kwetu sote. Aliegemea kifuani
pangu. Nilisikia harufu nzuri ya uturi aliofukiza kwenye
blauzi yake. Nikagundua kwamba sijamuangalia kwa
makini mke wangu kwa kipindi kirefu sana. Nikagundua
hakuwa binti tena. Kulikuwa na mikunjo usoni na
nywele zake zilianza kuwa nyeupe! Ndoa yetu imekula
urembo wake. Kwa dakika moja nikafikiri kwa nini
namfanyia hivi.
Siku ya nne nilipombeba hisia za mapenzi kati yetu
zilirejea. Huyu ni mwanamke aliyejitoa kuishi nami na
tumeishi kwa miaka kumi sasa. Siku ya tano na ya sita
ilikuwa wazi kwamba mapenzi yetu yalikuwa yakimea
upya. Sikumwambia Mary kuhusu jambo hili. Kadiri
mwezi ulivyokaribia kwisha niliona raha kumbeba mke
wangu na zoezi likawa rahisi zaidi. Pengine kufanya
kazi hii kila siku kuliniimarisha zaidi.
Alikuwa akichagua nini cha kuvaa asubuhi. Alichagua
mavazi kadhaa hakupata linalomfaa. Kisha akaguna,
‘nguo zangu zote zimekuwa kubwa’. Nikagundua
kwamba mke wangu amepungua sana, nadhani ndiyo
maana niliweza kumbeba kirahisi. Ghafla jambo
likanichoma... mke wangu ana uchungu na maumivu
makuu moyoni mwake. Bila kujitambua nikamgusa
kichwa chake. Mara mtoto wetu akatokeza na kusema
‘baba ni wakati wa kumbeba mama muende kazini’.
Kwake kumuona baba akimbeba mama likawa ni jambo
la furaha sana. Mke wangu alimuonyesha ishara
mwanetu asogee karibu na akamkumbatia kwa upendo
mkuu. Niligeuza uso wangu nisije nikabadili mawazo
katika dakika ya mwisho. Kisha nikambeba mikononi
mwangu kutoka chumbani, sebuleni halafu mpaka
mlangoni. Mkono wake laini ulikuwa umeizunguka
shingo yangu kwa upendo. Nilimkumbatia mwili wake;
ilikuwa ni mithili ya siku ya ndoa yetu. Lakini wepesi
wake ulinitia mashaka.
Siku ya mwisho nilipombeba nilipata shida hata kupiga
hatua moja. Mtoto wetu alishakwenda shuleni.
Nilimshika kwa karibu na kumwambia sikubaini kwamba
maisha yetu yalikosa upendo. Nikaenda zangu ofisini….
Nikashuka garini hata bila kufunga mlango. Maana
nilihisi nikichelewa tu ninaweza kubadili nilichoamua....
nikapand ngazi. Mary alifungua mlango nikamwambia,
‘Samahani, Mary, sihitaji tena kumtaliki mke wangu’.
Akaniangalia kwa kustaajabu, halafu akagusa kichwa
changu. Akaniuliza ‘Unaumwa?’ Nikaondoa mkono wake
kichwani kwangu. ‘Samahani, Mary, nimesema sitaki
kumtaliki mke wangu. Nadhani ndoa yangu haikuwa na
furaha kwa sababu sikuthamini undani wa maisha yetu,
mimi na mke wangu, si kwamba hatupendani.
Nimetambua hilo tangu nilipombeba siku ya ndoa yetu
nilitakiwa kumbeba siku zote za maisha yetu,
nampenda mke wangu sitamuacha mpaka kifo
kitakapotutenganisha.’
Ikawa kama Mary alizinduka usingizini. Akanizaba kibao
cha nguvu, akajiegemeza mlangoni na kuanza kulia.
Nikashuka ngazi na kuondoka zangu. Nikaingia kwenye
duka la maua nikaagiza maua mengi mazuri kwa ajili
ya mke wangu. Muuzaji akaniuliza aandike nini kwenye
kadi. Nikatabasamu na kuandika “Nitakubeba kila
asubuhi mke wangu mpaka kifo kitakapotutenganisha”.
Jioni ile nilifika nyumbani na maua mikononi mwangu,
tabasamu kubwa usoni nikakimbia mpaka chumbani,
nikapokelewa na maiti ya mke wangu kitandani.
Kumbe mke wangu alikuwa akisumbuliwa na saratani
kwa miezi kadhaa nami nilishindwa kubaini kwa sababu
nilihamishia akili yangu kwa Mary. Alijua kwamba
angekufa karibuni na alitaka asiniingize katika chuki na
mwanetu kama ningelazimisha talaka mapema.
Angalau machoni mwa mwanangu naonekana ni mume
mwema


Friday, 11 March 2016

KIJANA ULIYEKO ARUSHA NA SEHEMU NYINGINE, HII SIO YA KUKOSA.MWALIKE NA MWENZAKO

To All Youth / University/School Students,
NGO’s Practitioners,
Government Officials and Other Forward Thinking Individuals

RE: INVITATION TO ATTEND “TANZANIA NATIONAL YOUTH ASSEMBLY” FROM April 9th -10th 2016 at the SUNDOWN CARNIVAL HOTEL, ARUSHA TANZANIA.

Introduction

Enkisuma trust Fund is a company limited by guarantee that works to bring together the young generations brightest and best to ensure that their concerns, opinions and solutions are heard. It provides opportunities for young adults to join in a national and regional network of socially committed people with leadership potential, from there; they take action, driving positive change in their communities, companies and region in Tanzania and beyond.
The Summit will be facilitated by high profile counselors who have excelled in their various fields and range from politicians, activists, entrepreneurs, founders and CEOs to musicians, models and chefs. They advise, inspire, and celebrate the achievements of the forum's young ambassadors.
Enkisuma Trust and its partners in Tanzania and East Africa, are inviting all talented young people with vision, mission and passion in creativity at Politics, Entrepreneurships, Human rights, Education, environmental issues and sustainable development, in a Youth Transformational events that bring together talented youth Leaders across the country and East Africa, for training, empowering and networking them for sustainable future.
From the summit, young people shall be trained and advised the proper techniques to success in their fields of interests. Also, they shall share experience and opinion openly with the others for the purpose of making a better future for all.
Objectives of the Summit/Assembly
• To educate, enhance, network, inspire and empower Tanzania’s Youth to find solutions that eradicate youth unemployment, poverty, illiteracy and injustice.
• To enhance creativity skills that is important for the economic growth and personal development of the youth.
• To establish a network of young leaders that contributes to the welfare of Tanzania and Africa.
• To enhance, and sustain African Youth’s relationships through the empowerment of the participants.
• To enable youth to be able to contribute to civil society in Tanzania and Africa.
• To provide the youth with fresh insights and new perspectives that will deepen their understanding on entrepreneurship as a major tool for youth to creates Jobs.
• To help youth be part of building the Tanzania’s economic, political, cultural, religious, and social framework.
• To strengthen professional, economic, cultural, political, and scientific cooperation through close personal and professional relationships.
• Provide an avenue for the youth’s voices to be heard by the governments and the public in genaral.
Confirmed Facilitators and counselors that will lead to inspire Youth at the Assembly
1. Honorable Edward Ngoyai Lowassa, Tanzania retired prime minister
2. Antony Mavunte (MP) and Minister
3. Eric Shigongo, Author and CEO Global Publishers limited
4. Dr. Eliamani Laltaika, lecturer at Nelson Mandela University Arusha
5. Mr. Sheria Ngow, Fashion Designer and Entrepreneur
6. Maza Sinare, Entrepreneur
7. Patric Ngowi, Entrepreneur
8. Joshua Nasari (MP)
9. Antony Luvanda Entrepreneur
10. Niki wa Pili Musician and Entrepreneur
11. Mama Ndinini Kimasero CEO and Founder of MWEDO
12. Ruge Mutahaba Progamme director Clouds media

For more information about our counselors and their profiles go through our event website www.vijanaassembly.org
Expected outcome
The youth will be inspired, transformed and empowered to build meaningful confidence to commit in a changing world by starting their small enterprises and projects. They will also come up with solutions that will have a positive impact in the society.
Who will attend?
All talented young people in Tanzania and East Africa and committed individuals who have leadership ability and a commitment to effect positive change.
The summit will take place on 9th – 10th April 2016, in Sundown carnival, near to Arusha Airport, Arusha Tanzania.



Entrance fee;
1. The price per participant is Tsh 25,000 per plus VAT (where applicable). The price does not include any flights or other transportation to or from the Summit. The travel and accommodation costs for participant must be arranged independently by the participant sponsor or by the participant.
2. The Delegate price includes certificate of attendance, breakfast, lunch, Summit venue, Summit hand-outs and support materials for two days

Send your interest by mailing us at, info@vijanaassembly.org, info@enkisumafund.com or for more information go through the event website; www.vijanaassembly.org.
OR Call us direct through +255766075353 or +255758778540

Mbayani Tayai
On behalf of Tanzania National Youth Assembly organizing committee

New video: Mabibi na Mabwana Sauti sol na Alikiba wametuletea video ya unconditionally bae

BONYEZA HAPA KUUONA WIMBO WOTE

http://millardayo.com/sautimac11/


BABA MZAZI WA LULU YUPO TAYARI KWA MAHARI YA MWANAYE, MUDA WOWOTE



Nyota wa filamu hapa nchini Elizabeth Michael a.k.a Lulu baada ya kurudi Tanzania kwa ushindi wa tuzo kutoka Nigeria, hatimaye baba yake mzazi amefunguka na kusema kuna mtu mwenye mahari ya kumposa ili amuoe mwanaye basi na aipeleke.

Baba yake Lulu ameongea na E-newz na kutufahamisha bado hajapokea mahari ya mwanae na yupo tayari kupokea mahari, hivyo E-news imeamua kuutoa ujumbe huu wa baba Lulu.

Huku wengi wakidhani kuwa ujumbe huo unaweza kumfikia mtu mzima Majey ambaye kwa sasa wapo kwenye mahusiano na Lulu.

Korea Kaskazini yaamrisha majaribo zaidi ya mabomu



Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-Un ameamrisha majaribio zaidi ya kinyukilia yakitumia mabomu yasiyokuwa na nguvu, ambayo anasema wanasayansi wa nchi yake wametengeneza.

Shirika la utangazaji nchini limetangaza kwamba Kim alitoa amri hiyo baada ya kushuhudia uzinduzi wa makombora mengine hapo Alhamisi.

Awali kiongozi huyo alisema wanasayansi wa nchi yake wamefanikiwa kupunguza ukubwa na mabomu ili yaweze kuwekwa kwenye makombora.

Waandishi wa habari wamesema ikiwa hili litathibitishwa, hii itakua tishio kubwa kwa Korea Kusini na nchi nyingine zilizoko kwenye kanda hiyo.


MBUNGE ACHEZEA KICHAPO TOKA KWA MKEWE HADI KULAZWA

UKATILI WA KIJINSIA?


Mwanasiasa mkongwe Moses Wetang’ula Senator wa kaunti ya Bungoma, ambaye pia ni Waziri wa zamani wa mambo ya nje na Waziri wa zamani wa Biashara nchini Kenya. Jumapili ya tar.6 March (siku mbili kabla ya kuadhimisha siku ya wanawake duniani) alipewa kipigo kikali na mke wake An Wacheke Ngugi hali iliyopelekea kukimbizwa hospitali kwa matibabu kabla hajaenda kuripoti Polisi ambapo alikuta mkewe ameshamtangulia kuripoti. Yani mke alimpiga mume kisha akawahi Polisi kusema amepigwa.


Hali hiyo ilipelekea kutengenezwa kwa picha hii na wapinzani wake kisiasa (photoshop) wakionesha alivyoathiriwa na kipigo cha mkewe. Licha ya kuwa picha hii ni photoshop lakini ni kweli kuwa Wetangula alipigwa na mkewe na kupatiwa matibabu ktk hospitali ya Bungoma.


Gazeti la Daily Nation la nchini Kenya limeripoti kuwa hii si mara ya kwanza kutokea mafarakano na kupigana kati ya Wetangula na mkewe Ann. Licha Ann kutoa kipigo hicho kwa mumewe lakini na yeye amekimbilia Polisi kumshtaki Wetangula. Kesi hii ni ya pili baada ya ile aliyofungua February 18 akidai kupigwa tena na mumewe.


Ann Wacheke Ngugi ni mfuasi wa muungano wa vyama vya siasa vya Jubilee Alliance vinavyoongoza serikali chini ya Rais Uhuru Kenyatta, licha ya kuwa mumewe ni kiongozi wa chama cha upinzani cha CORD. Tofauti ya kisiasa ya wenzi hao wawili inasemekana kuwa chanzo cha mfarakano ndani ya ndoa yao.


Kumekuwa na desturi kwa wanasiasa wengi nchini Kenya kupokea kipigo au kufanyiwa unyanyasaji wa kijinsia na wake zao. Rais Kibaki na Arap Moi ni miongoni mwa viongozi wa juu wa nchi hiyo waliodaiwa kupigwa na wake zao. Wetangula pia ametangaza nia ya kugombea Urais mwakani. Ikiwa atapitishwa na chama chake na kushinda bila shaka ataendeleza list ya Marais wa Kenya kupigwa na wake zao. Je ingekua wewe ndo Wetangula ungefanyaje??


TANGAZO KUTOKA TAMISEMI

TAARIFA KWA UMMA 

Kumekuwa na taarifa za upotoshaji zinasombazwa kwenye mitandao ya kijamii juu ya kutolewa kwa ajira mpya ya walimu kwa shule za sekondari na msingi kwa mwaka 2016/2017.


Taarifa hizo zinazosambazwa zinaeleza kwamba walimu wapatao 17,928 wa cheti (Daraja IIIA) , 5,416 wa Stashahada kwa sekondari na 12,677 kwa shule za mazoezi za vyuo vya ualimu Tanzania Bara wamepangwa kwa ajili ya kuanza kazi.


Katika taarifa hiyo inawataka walimu hao waliopangwa kuripoti kwa Wakurugenzi wa Halmashauri kwa ajili ya kupangiwa vituo vya kazi na kuanza kazi tarehe 01/04/2016.


Taarifa hizo pia zinaeleza kuwa walimu ambao hawataripoti ifikapo tarehe 10/04/2016 hawatapokelewa tena na watakuwa wamepoteza ajira zao.


Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) inapenda kuchukua nafasi hii kukanusha taarifa hizo kuwa ni za upotoshaji. Wananchi wanapaswa kuzipuuzia kwani mpaka sasa bado Serikali haijatoa ajira za walimu kwa mwaka 2015/2016.


Ajira mpya za ualimu zitakapokuwa tayari zitatangazwa moja kwa moja kwenye vyombo vya habari na katika tovuti ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI ambayo ni www.tamisemi.go.tz.


Imetolewa na :
Kitengo Cha Mawasiliano Serikalini
Ofisi ya Rais
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
11/03/2016

J E S A M BLOG SPOT.COM: MAGUFULI ANAYO MAJINA YA WAFANYAKAZI HEWA BENKI KUU, SOMA MAAGIZO MAZITO KWA GAVANA

J E S A M BLOG SPOT.COM: MAGUFULI ANAYO MAJINA YA WAFANYAKAZI HEWA BENKI KUU, SOMA MAAGIZO MAZITO KWA GAVANA

MAGUFULI ANAYO MAJINA YA WAFANYAKAZI HEWA BENKI KUU, SOMA MAAGIZO MAZITO KWA GAVANA

" Yako majina mengi humu, sitaki kuyataja mengine hapa, au niyataje yote? Muyafute yote majina ya watu ambao sio wafanyakazi wa BOT. Mbaki na watu wanaofanya kazi ili mshahara uende kwa watu wanaofanya kazi tu. Nina orodha yote, ninaijua yote." - Amesema hayo Rais Magufuli jana wakati alipowaweka kitimoto viongozi wa BOT kulipa mshahara majina ya watu wasiofanya kazi.

MBOWE: NAWALETEA KATIBU MKUU MAKINI SANA

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amevunja ukimya na kusema atawasilisha jina makini la mrithi wa nafasi ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa.


Akizungumza na MTANZANIA mjini hapa jana, baada ya kumalizika kikao cha kwanza cha Kamati Kuu, Mbowe alisema sifa za kiongozi anayepaswa kushika wadhifa huo zinafahamika.


Alisema wajumbe na wanachama wa Chadema watarajie kumpokea mtu makini ambaye jina lake atalipendekeza kisha kupigiwa kura na wajumbe wa Baraza Kuu kesho.
“Sifa za Katibu Mkuu zinajulikana, nawaomba wanachama na wajumbe kutulia, jina watakutana nalo ukumbuni muda ukifika… nina imani litakuwa jina la mtu makini,” alisema.


Mbowe alisema chama hicho kinakutana kwa mara ya kwanza tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa Rais mwaka jana, hivyo wana mambo mengi ya kujadili, ikiwa ni pamoja na kupanga mikakati mipya ya kuwafikia wafuasi wao.


Katika hatua nyingine, chama hicho kimesema kitamtambulisha Katibu Mkuu mpya rasmi Jumapili wakati wa mkutano wa hadhara utakaofanyika viwanja wa Furahisha jijini hapa.


Akizungumza na waandishi wa habari jana, Ofisa Habari wa chama hicho, Tumaini Makene, alisema majina mawili yatawasilishwa katika Baraza Kuu litakalokaa usiku wa Jumamosi kwa ajili ya kupitisha jina moja.


Alisema majina yatakayowasilishwa hayatakuwa na uhusiano au urafiki wowote na Mwenyekiti Mbowe.


“Tayari viongozi wa kitaifa wamewasili Mwanza, Sekretarieti imekutana kwa ajili ya kuandaa ajenda ambazo zitajadiliwa na Kamati Kuu yenye wajumbe 36.


“Siku inayofuata Baraza Kuu litakaa usiku kwa ajili kumpata Katibu Mkuu, hii ni nafasi nyeti sana ndiyo maana hata wenzetu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanafuatilia kwa ukaribu kujua nani atapewa mikoba ya Dr Slaa.

MBUNGE NA KATIBU WAKE WAHOJIWA ZAIDI YA SAA TATU HUKO MBEYA

Mhe.Pascal Haonga amehojiwa na police kwa muda wa saa mbili....

.....mbunge huyo anashtakiwa kwa kosa la kuharibu mali hii ni baada ya mbunge akishilikiana na wananchi kuondoa kizuizi cha mazao kilichowekwa na halmashauli kwa ajili ya ushuru wa mazao kuazia debe 1 na kuendelea kwa kila kata.

vizuizi hivyo vimekuwa kero kubwa kwa wananchi kwenye jimbo lake kitendo ambacho wananchi wamekuwa wakilalamika kila wakati kwa muda wa miaka mingi,MHE.Haonga aliwaahidi wananchi hao wakati wa kampeni wakimchagua kuwa mbunge atahakikisha kufuatilia sheria ya uanzishwaji wa vizuizi hivyo maana kama ni ushuru wakulima ususani wa kahawa hulipa asilimia 5% KWA KILA kilo.


EMPLOYMENT OPPORTUNITY-MERERANI

Job Title: Accountant
Organization: Tanzanite One Mining Limited (TML)

Company Profile:
Tanzanite, a blue/violet gemstone variety of zoisite is only produced in NE Tanzania. TML owns the mining license for Block C-a significant portion of the only known Tanzanite producing resource, located in the follthills of Mt Kilimanjaro, Tanzania. TML is operating an Underground Mine and a Plant at Mererani-Simanjiro Manyara Region, Tanzania.

Job Brief
We are looking for an accountant to professionally handle accounting data in order to provide quantitative information.

Responsibilities
• Manage accounting operations based on accounting principles.
• Be an excellent team player on month-end and year-end close process.
• Collect, analyze and summarize account information.
• Compute taxes and prepare tax returns.
• Develop periodic reports for management.
• Audit financial transactions and document accounting control procedures.
• Keep information confidential and secure them with random database backups.
• Keep up with financial policies, regulation and legislation.

Eligibility Criterion
• Proven work experience of not less than 4 years in accounting and/or audit or relevant field.
• Thorough knowledge of accounting and audit principles and procedures.
• Excellent accounting software user especially pastel evolution.
• Strong attention to detail and confidentiality.
• Advanced degree in Accounting, CPA or ACCA will be an added advantage.

Location: Tanzanite One Mining Limited, Mererani Simanjiro Manyara Region, Tanzania.

How to Apply
Interested candidates may send their CV with three referees to: hr@tanzaniteone.com and/orsaitoti@tanzaniteone.com before 18th March 2016.

Tanzanite One Mining Limited
P.O.BOX 15237
MERERANI

Only shortlisted candidates will be contacted.

Source: Mwananchi 10th March, 2016

UNATAFUTA KAZI? KAMATA FURSA NA NACTE,NAFASI MBICHI KABISA

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA (NECTA)
VACANCIES

The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) is a Government Agency which is under the Ministry of Education, Science, Technology and vocational. NECTA was established by the parliamentary Act No.21 of 1973 to undertake the responsibility of administration of National Assessments/Examinations and other functions as provided for in the Act. The aim of NECTA is to contribute to National development through a fair, efficient and effective National Examinations and Educational Assessment system that provides high quality stakeholders service through competent and motivated staff.
NECTA invites applications from Tanzanians who are suitably qualified dynamic and results oriented to fill the following vacancies.
Job Title: Examinations Officer II (1 post)

Qualifications
• Holder of Bachelor of Science with Education majoring in Chemistry from a recognized Institution and must be computer literate and fluent in English and Kiswahili.

Duties and Responsibilities
• Coordinates setting and moderation of examinations items and marking schemes.
• Typeset examination papers and marking schemes.
• Proofreading question papers, marking schemes and various reports related to examinations.
• Updates inventory of examiners.
• Compiles lists of examiners for various examinations.
• Supervises marking of examination papers.
• Compiles estimations of materials required at marking centres.
• Carries out post facto analysis of subjects examined by NECTA for the purpose of providing feedback to schools and other stakeholders.
• Compiles lists of candidates who appeal against the National Examinations results.
• Performs any other duties relevant to the functions of NECTA as assigned by his/her superiors.
=========

Job Title: Examinations Officer II 1 post)

Qualifications
• Holder of Bachelor of Science with Education majoring in Biology from a recognized Institution and must be computer literate and fluent in English and Kiswahili.

Duties and Responsibilities
• Coordinates setting and moderation of examinations items and marking schemes.
• Typeset examination papers and marking schemes.
• Proofreading question papers, marking schemes and other various reports related to examinations.
• Updates inventory of examiners.
• Compiles lists of examiners for various examinations.
• Supervises marking of examination papers.
• Compiles estimations of materials required at marking centres.
• Carries out post facto analysis of subjects examined by NECTA for the purpose of providing feedback to schools and other stakeholders.
• Compiles lists of candidates who appeal against the National Examinations results.
• Performs any other duties relevant to the functions of NECTA as assigned by his/her superiors.
=========

Job Title: Office Assistant II (1 post )

Qualification
• Holder of CSEE with a pass in English and Kiswahill.

Duties and Responsibilities
• Careful handling of files and other official documents to respective offices.
• Cleans Offices.
• Makes arrangements of furniture and equipments in offices/halls.
• Keeps safe custody of office property where required.
• Collects and delivers mails.
• Performs any other duties relevant to the functions of NECTA as assigned by his/her superior.

Other Attributes
In additional to the qualifications specified under each post, all applicants are expected to possess the following attributes.
• High integrity, quick to learn and adapt.
• Capacity to work under pressure and meet strict deadlines.
• Excellent interpersonal and communication skills.
• Knowledge and skills in computer applications.
• Age not exceeding 45 years.

Remuneration
Salary for each post and other incentives will be offered based on NECTA`s salary scales.

Mode of Application
Employ applicants should channel their application letters through their employers. Properly word-processed CVs, names and contact addresses of three referees, and copies of all academic certificates and transcripts must be attached. A recent passport size photograph of the applicant must be affixed on the top centre of the application letter. Applicants should provide their complete contact address, including telephone numbers and e-mail addresses. Applications should be sent to the following address before 08th April, 2016 at 3:30pm.
Only short listed applicants will be contacted.

The Executive Secretary
National Examinations Council of Tanzania
P.O.BOX 2624
DAR ES SALAAM
Tel: +255 22 2700493/6 Fax: +255 22 277596
Email: esnecta@necta.go.tz

Please note: Submission of forged or unlawfully possessed certificates including cheating of whatever nature will be strictly dealt with according to the provisions of the laws.

Source: Daily News 10th March, 2016

TWENDA ZETU KWA OBAMA,SOMA NA OMBA NAMNA YA KUNUFAIKA NA MRADI WA VIJANA WA AFRICA TOKA SERIKALI YA MAREKANI


NAFASI ZA KAZI MPYA KABISA






Job Vacancy > Assistant Lecturer-Economics (Re-advertised)

Location > Morogoro 

Position Type > Full Time 

Organization Type >Government










Sokoine University of Agriculture



















Application Deadline: 24 Mar 2016




ASSISTANT LECTURER-ECONOMICS (RE-ADVERTISED) POSITION DESCRIPTION:







From The Guardian, 10th March 2016

The Management of Sokoine University of Agriculture (SUA) invites suitable qualified Tanzanians to apply for positions of Tutorial Assistant and Assistant Lecturer.




POSITION: Assistant Lecturer (3 positions)




Duties and Responsibilities

a) To carry out lectures, conduct tutorials, seminars and practicals for undergraduate programmes;

b) To prepare and present case studies;

c) To conduct and publish/disseminate research results;

d) To recognize students having difficulties, intervene and provide help and support;

e) To participate in consultancies and community services under supervision;

o To attend workshops, conferences and symposia; and

g) To perform any other duties that may be assigned by the relevant authorities.

Age: Not above 45 years of age







Remuneration:

As per Treasury Registrar's Circular NO.7 of 2015, which is applicable at the moment.




DEPARTMENT OF BIOMETRY AND MATHEMATICS (1 position)

Discipline: Economics




Qualification:

Possession of a Bachelors degree with a minimum GPA of not less than 3.8 out of 5 and a Masters degree with a GPA of not less than 4.0 out of 5 in Economics.













APPLICATION INSTRUCTIONS:







Please Note:-

Only shortlisted candidates will be contacted through their addresses e-mail and/or telephone

Those who applied for similar posts in the past are encouraged to apply.

Those working in the Public Service are required to route their applications through their current employers.

During application the applicant should state the Department, Position and Discipline one is vying for.




All applications should be addressed to the




Deputy Vice Chancellor (Administration and Finance),




P.O. Box 3000,




CHUO KIKUU,




MOROGORO










two weeks from the date of this advertisement. The application letters should indicate names and addresses of three referees, together with certified copies of certificates and transcripts, curriculum vitae and testimonials. 





Job Vacancy > Accountant
Location > Zanzibar 
Position Type > Full Time 
Organization Type >Company Website >http://www.hrmafrica.net

HRMAfrica 








Application Deadline: 30 Mar 2016
ACCOUNTANT POSITION DESCRIPTION:





Our client: A luxurious beach hotel situated on one of the most beautiful beaches of Zanzibar and offers top of the industry luxurious accommodation is seeking qualified person to fill the following vacancy;

ACCOUNTANT

Description

At least 2 years’ experience in the hotel or related industry

Degree/Advance diploma in accounting

CPA will add advantage

Aware of accounting packages especially quick books and tally

Excellent in excel, report writing and presentation skills






APPLICATION INSTRUCTIONS:





academic certificates,professional certificates, cv and cover letter via the website above.




HUMAN RESOURCE MANAGER POSITION DESCRIPTION:


Follow the Instructions on the website:
http://www.hrmafrica.net/


Featured post

MWANAMKE YAFUATE HAYA; NI MUHIMU KWA MAHUSIANO YAKO

1. Degree yako ya fist class uliyoipata chuo kikuu haiwezi kukufanya uwe mke first class katika ndoa yako bali ni heshima yako na uthubu...