Tuesday, 25 April 2017
SOMA HAPA UELIMIKE KUHUSU NDOA
NDOA NI KAZI NGUMU,HAIHITAJI MCHEZO!!!
Nimezoea kutafsiri kwamba "ndoa sio kwa ajili ya wavulana wadogo" nikimaanisha wavulana wadogo kiumri, ni mpaka pale nilipomtembelea bibi mshauri wa masuala ya mahusiano aliyedumu ktk ndoa kwa miaka 47.
Nilimuuliza nini siri ya mafanikio ya ndoa yako kudumu miaka yote hiyo 47? Alijibu binti yangu, matarajio unayoyaweka juu ya ndoa yako yanweza kuharibu au kustawisha ndoa yako. Niliolewa na mume wangu bila ya matarajio ya kufurahia pesa na utajiri wake, au kuninunulia motokaa.
Ila kadiri muda ulivokua ukisonga, uvumilivu wangu, uchapaji kazi, hofu ya Mungu vilipelekea kupata utajiri, nyumba kadhaa, watoto wenye afya na mengineyo
Unaona? Kama mwanamke utaendelea kulalamika ndani ya nyumba, unasukumua spirit ya mwanaume kutofurahia uwepo wake nyumbani, kama hutamfurahisha mumeo unatengeneza nyumba isiyotawalika.
Hivyo basi niliolewa pasina matarajio makubwa sana, ila nilijitahidi kumtengenezea furaha siku zote kadiri nilivyoweza. Kwa miaka yote 47 nimekuwa wa kwanza kuamka na wa mwisho kwenda kulala.
Naogesha watoto, nawaongoza ktk sala, naandaa breakfast kwa ajili ya mume wangu na watoto na kumchemshia maji ya kuoga, namnyoshea nguo za kazini, namkiss na kumtakia heri kazinj na mizunguko yake yote ya siku.
Nikamuuliza bibi, kwa kufanya hayo yote ulikuwa unapata mrejesho gani mzuri toka kwa mumeo? Akacheka na kuniambia; unaona! Hili ndio tatizo kubwa nyie mabinti wa siku hizi katika ndoa. MNAFANYA KITU KWA KUTEGEMEA NAWE UTAPEWA FADHILA KUTOKA KWA MWENZI WAKO. Hiyo sio sahihi. Kama tabia ya kumhudumia mpenzi wako ikijijenga, naturally utapata mrehesho kutoka kwa mwenzako.
Akaendelea, binti yangu kamwe usifikirie kuhusu utajiri au umasikini wa nyumbani ulikotoka na ukafananisha ktk ndoa yako. Hata hivyo umejua kabisa status ya familia yako na ukaamua kuoa au kuolewa na huyo mtu. Mapenzi ndio huvutia wawili kuingia ktk ndoa, ila si mapenzi pekee bali ni uelewa, uvumilivu, mawasiliano na muhimu zaidi n msamaha.
Matarajio makubwa ktk ndoa ni dalili ya kuvunjika kwa ndoa mapema. Muda mwingine utasikia nataka kuolewa/kuoa na mfanyabiashara, tajiri, mpole, asiye na dosari etc...huwezi kuvipata vyote hvyo kwa mtu mmoja ila kulingana na muda unaweza ukamtengeneza. Punguza matarajio makubwa.
Mambo haya yafuatayo yaepukwe kwa gharama zozote na wanandoa!
1) Kamwe usiseme umemtengeneza mumeo au mkeo from nobody ti somebody. Inaumiza. Mungu amekutumia wewe kama wakala tu wa kumbadilisha. Mpe utukufu yeye.
2) Muache mwanaume awe kichws cha nyumba, na wewe mwanamke kuwa roho ya nyumba huku ukitumia ulimi wako vizuri!
3) Tendo la ndoa ni chachu ya kuimarisha ndoa, jitahidi kuwa romantic kwa mwenzi wako.
4) Mtegemee zaidi Mungu kudumisha ndoa yako na si wanadamu katika kutatua migogora ya hapa na pale
5) Mwanamke usitumie muda mwingi kuweka make up ya mwili wako, bali make up ya tabia zako ndio ipewe kipaumbele.
Fanya kila jitihada kufanya ndoa yako idumu na Mungu atusaidie.
Amen.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Featured post
MWANAMKE YAFUATE HAYA; NI MUHIMU KWA MAHUSIANO YAKO
1. Degree yako ya fist class uliyoipata chuo kikuu haiwezi kukufanya uwe mke first class katika ndoa yako bali ni heshima yako na uthubu...
-
Kuna wakati fulani niliamua kwenda dukani pale mijini Dodoma katika duka la mfanyabiashara mmoja maarufu sana.Lengo la kwenda pale liliku...
-
Mithali 14: 1 “Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe”. Padre m...
-
Job Title: Accountant Organization: Tanzanite One Mining Limited (TML) Company Profile: Tanzanite, a blue/violet gemstone variety of zoisit...

No comments:
Post a Comment