Barua kwa wasichana wote
Dear Ladies
Sio kila mwanaume ni Husband material. Baadhi yao wanafaa kuwa marafiki tu, baadhi yao ni boyfriend materials, sex mate materials,baby papa materials, husband materials na wengine ni husband materials.
Olewa na mwanaume ambae ni Kaka bora, mume bora na baba bora. Baadhi yenu huingia ktk ndoa na wanaume ambao kimsingi hawakua na nia ya kuoa.
Ndoa si kwa kila mtu. Baadhi ya wanaume kimsingi hawajawa tayari na majukumu ya ndoa. Kamwe usiruhusu kiu ya ndoa au msukumo wa marafiki na wanajamii kwa ujumla ukusukume kuingia mikononi kwa mwanaume ambae hayuko tayari na ndoa (matrimony).
Tizama kwa makini, wanaume wengi huoa kwa sababu ya status. Hawa ndio huoa na kuwachia mama zao na baba zao wawatunzie wake zao.
Namaanisha nini?
Usikubali kuolewa kwa nadharia, ndoa njema lazima ihusishe vitendo vyenye kuleta uhai wa ndoa. Baadhi ya wanaume ni wabinafsi sana, Chukua hii kutoka kwangu mwanaume mbinafsi hawezi kuwa mume bora.
Ndoa huchanua pale panapokua na muingiliano wenye kuleta manufaa, humea pale panapokua na give-and-take situation.
Usiolewe na mwanaume kwa kuwa una mimba yake.
Usiolewe na mwanaume kisa anakufurahisha.
Usiolewe na mwanaume kwa sababu huna ajira.
Usiolewe na mwanaume kwa sababu umekua nae ktk uhusiano kwa muda mrefu.
Usiolewe na mwanaume kwa sababu umejiwekeza kwake kiuchumi
OLEWA nae kwa sababu umemchunguza kwa makini na umejiaminisha kwamba anafaa kuwe mume bora na baba bora wa watoto wako.
Wanaume wapo kila mahali, ila waume bora niwachache sana.
Nakuombea wewe ambae bado hujaolewa kwamba hutakabiliwa na ndoa yenye majeraha. Na kwa wale ambao wanajuta kufanya makosa ya kuchagua na wapo ktk majeraha mazito, Mungu aingilie kati ndoa zenu.Mungu wetu ni muanifu, atatenda vile aonavyo yeye ni vema!
No comments:
Post a Comment