Friday, 10 June 2016

HATUA SABA MUHIMU ILI KUWA MJASIRIAMALI MWENYE MAFANIKIO


Ujasiriamali ni neno la kiswahili linalotokana na maneno mawili yafuatayo
1.    Ujasiri 2.
2.    Wa mali
Hii ina maana ya mtu mwenye ujasiri wa kuwekeza mali alizonazo ili apate faida
 Hatua 7 muhimu ili kuwa mjasiriamali kamili (J7)
1. Jitoe bila woga na kuwekeza ulicho nacho
2. Jipange (mpango mkakati)
3. Jipime Ili kujua uwezo na madhaifu yako
 4. Jiwezeshe kwa kupata mafunzo
 5. Jihadhari ili usitumbukie kwenye hatari
 6. Jitadhmini, jikosoe kwa kujitathmini
 7. Jipange upya kwa kufanya maboresho


1. Jitoe Bila Woga na Kuwekeza Ulicho Nacho.
Maamuzi magumu yanatakiwa unapotaka kuwa mjasiriamali. mke, mume, wazazi, wajomba ndugu, marafiki, wakuu wa ukoo wako na hata mazingira yako yanaweza kukataa au kuwa pingamizi kubwa ili usifanye shughuli za kijasiriamali. Kwa mazingira haya ni rahisi kukata tamaa na kama hukuamua kutoka moyoni mwako fikra zako za kuwa mjasiriamali zitaishia hapo na hutakaa ufanye biashara. Kuamua na kujitoa ni muhimu sana ili uweze kuendelea an maono yako yatakayokukomboa kiuchumi Ili uweze kujenga himaya yako (ufalme wako) (your kingdom) wa utajiri unahitaji kufanya maamuzi yako peke yako wala sio ya hao waliotajwa hapo juu japo ushauri kutoka kwao ni ruksa na utakusaidia kufanya maamuzi bora zaidi. Kujitoa unakusaidia wewe kuhesabu gharama ya hatari zitakazokuwepo mbele yako kwenye ujasiriamali wako. Utahitajika saa nyingine kuwekeza mali ya kipekee uliyonayo. kama vile nyumba, gari, kiinua mgongo nk. Kama wewe ni mwoga hutadhubutu kuwekeza kajumba kako ka­pekee eti kwa sababu ya ujasiriamali. Kama kweli ukiamua na kujitoa maisha yako yatabadilika sana kuanzia siku ile ya maamuzi magumu. Safari ya ujasiriamali huwa na tabia ya kwenda juu au chini kama meli inayoyokabiliana na tufani baharini. Unashauriwa kutizama lengo na sio tufani ya bahari. Kama umeamua kutoka moyoni kuwekeza utafika tu kwenye lengo kuu. Epuka kukopa ili uanzishe biashara, ni hatari sana. Kusanya vyazo vyako vya mitaji (mali binafsi )

 2.Jipange (Mpango Mkakati)
 Weka maono ya biashara yako, unataka kufikia ngazi ipi kimafanikio. Je unataka kuwa na hoteli kubwa ya kitalii au kiwanda kikubwa cha kuuza nguo Tanzania au Afrika nzima? Weka na kazi muhimu utakazozifanya ili kufikia maono husika. Unaweza weka malengo mahsusi kila baada ya miaka mitatu au mitano. Inashauriwa malengo hayo mahsusi yawe kati ya 3 na 5. Jiwekee malengo ya muda mrefu na muda mfupi. Malengo yagawanywe mpaka kwenye kazi za kila siku. Jiwekee maadili na tunu za mafanikio. Bila hizi tunu na maadili huwezi kuyafikia malengo yako. Jiwekee ratiba mbalimbali za kiutekelezaji bila kusahau kuweka kwenye ratiba shughuli muhimu.
3. Jipime Ili Kujua Uwezo na Madhaifu yako Kiingereza wanaita SWOT Analysis
 Jipime juu ya mambo makuu manne yaliyogawanyika kwenye makundi mawili
 1. Mazingira ya biashara ya ndani
 2. Mazingira ya biashara ya nje
 AU
 1. Mazingira wezeshi
2. Mazingira hatarishi
Haya makundi mawili nayo yamegawanyika katika Mazingira ya ndani ni
 1. Uwezo wako kibiashara
 2. Udhaifu wako kibiashara
 Mazingira ya nje ni
 1. Fursa zilizopo ili kunufaisha biashara yako
2. Hatari zilizopo ili kuua biashara yako
 Mazingira wezeshi ni kama ifuatavyo
1. Fursa zilizopo ili kunufaisha biashara yako
 2. Uwezo wako kibiashara Mazingira hatarishi ni kama ifuatavyo
 1. Hatari zilizopo ili kuua biashara yako
2. Udhaifu wako kibiashara unaoweza kuzorotesha maendeleo ya biashara yako
4. Jiwezeshe kwa Kupata Mafunzo
 Jiwezeshe ni hatua inayojibu matokeo ya hatua ya kujipima ambayo imekuwezesha kugundua madhaifu yako na kuyapatia ufumbuzi kwa kujiwezesha ambazo mara nyingi ni mafunzo. Udhaifu ni yale mambo ya kimaarifa usiyoyajua kiutendaji ili biashara yako isonge mbele. Inaweza kuwa ni ujuzi wa kufuga samaki kama unataka kuanzisha mradi wa kufuga samaki nk.
5. Jihadhari ili Usitumbukie Kwenye Hatari
 Katika hii hatua hakikisha kila uamuzi au tendo unalofanya halitakuingiza kwenye hatari kubwa usiyoweza kumudu bali inakuweka kwenye changamoto ambazo unazimudu. Kingereza wanaita (Moderate Risk). Usijaribu kufanya biashara zenye hatari kubwa na ya uhakika. Usijaribu kuingia ubia/ushirika na watu ambao unawajua ni hatyari kwa biashara zako. Usijaribu kuingiza teknolojia kwenye biashara yako ambayo una uhakika kuwa sio rafiki.
6. Jitadhmini,
 Jikosoe kwa Kujitathmini. Fanya tathmini za mara kwa mara ili kujua kama unakwenda sawasawa na makusudio ya mwanzo. Fanya tadhmini ndogo kila baada ya nusu mwaka, na tadhmini kubwa kila baada ya miaka mitatu.
 7. Jipange Upya kwa Kufanya Maboresho
 Matokeo ya tadhmini yatumike kama msingi wa kujipanga upya na kufanya maboresho makubwa yatakayoitoa biashara yako kutoka kwenye ngazi moja ya mafanikio kwenda ngazi ya juu zaidi ya mafanikio. Tumia matokeo ya tadhmini zote mbili kujikosoa na kufanya maboresho yenye lengo la kujibu kasoro zilizoonekana kwenye ripoti ya tadhmini.

Karibu tuendelee kujifunza zaidi

Mmassy Jerome-Arusha,Tanzania


No comments:

Post a Comment

Featured post

MWANAMKE YAFUATE HAYA; NI MUHIMU KWA MAHUSIANO YAKO

1. Degree yako ya fist class uliyoipata chuo kikuu haiwezi kukufanya uwe mke first class katika ndoa yako bali ni heshima yako na uthubu...