Friday, 10 June 2016

KANUNI ZA UJASIRIAMALI ZINAZOMWEZESHA AFANIKIWE


Kanuni za ujasiriamali zinaweza kusomwa au kufundishwa na mtu akaelewa na kuzifuata,lakini  tabia  zingine  hazifundishiki hizi ni zile tabia ambazo mtu anazaliwa nazo. Kila binadamu anauwezo tofauti katika kufikiri,kufanya maamuzi,kufanya kazi kwa bidii,tofauti hizi ndizo ambazo haziwezi kufundishika. Jambo la kutia moyo ni kwamba tabia ambazo zinafundishika ni muhimu sana kwa mjasiriamali au mtu yeyote anayetaka kufanikiwa katika biashara. Zifuatazo ni kanun muhimu  za ujasiriamali.
1.       Kuthubutu
hii ni tabia muhimu sana kwa mjasiriamali,hapa tunazungumzia uwezo na utayari wa kufanya maamuzi ya kuingia katika biashara fulani au mradi fulani huku ukiwa umeondoa nidhamu ya woga. Watu wengi ni waoga wa kuchukua hatua au kuthubutu kuingia katika biashara,mradi n.k,watu wanaogopa hasara,hawajui jinsi ya kuendesha mradi weyewe. Mtu ili aitwe mjasiliamali ni lazima awe na uwezo wa kuhtubutu kufanya jambo, lakini jambo atakalo thubutu kufanya lazima afanye utafiti wa kutosha il baadaye limletee tija. Waswahili mwanasema” UWOGA NI UMASIKUNI”.
2.       Nidhamu
Hii pia ni kanuni muhimu sana kwa mjasiriamali,mjasiriamali lazima awe na na nidhamu katika biashara yake,awe na nidhamu katika matumizi yake ya pesa na ni lazima awe na nidhamu ya kufanya kazi kwa bidii.nidhamu ni chanzo ch mafanikio. Mfano mfanyabiashara wa duka ni lazima awe na nidhamu kwa wateja wake ili wasimkimbie.
3.       Umakini na uelevu
Wale waliofanikiwa sio tu walikuwa tayari kufanya kazi bali waliweka umakini mkubwa katika kazi waliyokuwa wakifanya. Mjasiriamali anatakiwa kuwa makini kwa kila jambo,anatakiwa kujua soko linaendaje na pia ni lazima awe muelevu wa kutambua mabadiliko yanayojitokeza katika soko ,uzalishaji na uendeshaji kwa ujumla.
4.       Kuwa na uwezo wa kuongoza
Mjasiriamalia lazima awe na uwezo wa kuongoza na kutoa maamuzi. Baadhi ya watu wanadai uongozi  ni karama ombayo mtu anazaliwa nayo au anapewa na Mungu,ni kweli mtu anaweza kuzaliwa na kipaji cha kuongoza,lakini mtu anaweza kujifunza na akawa kiongozi mzuri. Katika ujasiriamali uongozi ni jambo muhimu sana,mjasiliamli lazima aweze kuongoza biashara yake au mradi wake vizuri. Mjasiriamali lazima awe na uwezo wa kusimamia wafanyakazi na kutumia mbinu  za uongozi ili apate matunda kwa kile ambacho anafanya.
5.       Kupenda kufanya kazi (kufanya kazi kwa bidii na maarifa)
Kitu kikubwa  hapa ni lazima mjasiriamli awe anaipenda kwa dhati shughuli anayofanya hii itamsaidia kufanya kazi kwa moyo.Kama unapenda kazi unayo fanya basi kazi hiyo haitakuwa mgumu,bali utakuwa unafanya kitu ambacho kwako ni hobi na mwisho wa siku utafanya kazi kwa bidii na maarifa. Watu waliofanikiwa ni wachapakazi.hivyo ni muhimu kuwa na tabia ya kufanya kazi kwa bidii.
6.       Uaminifu na ukweli
Hii nayo ni tabia ambayo mjasiriamali anatakiwa kuwanayo,wateja wengi wanapenda mtu mwamifu na mkweli. Kama mjasiriamali ni lazima ufanye kazi yako katika mazingira ya uaminifu na ukweli ili upate wateja wengi,lazima uwe mkweli katika bei  zako. Uongo katika biashara ni sumu ambayo itaua biashara yako mapema sana
7.       Dhamira
Mtu yeyote naweza kujiita mjasiriamali lakini kiukweli mafanikio yanahitaji uelewa wa kutosha,kufanya kazi kwa bidii huku ukiwa umeweka mbele lengo au dhamira. Lengo au dhamira ni motisha tosha itakaoyo kupa msukumo mpaka kufikia mafanikio. Dhamira ya kweli inahijajika kabla hujaingia katika biashara au mradi fulani.
8.       Kwenda na wakati
Mjasiriamali lazima aende na wakati ili aweze kutambua mabadiliko mbalimbali yanayo jitokeza katika masoko na uzalishaji wa bidhaa kwa ujumla. Kwenda na wakati hakutampa nafasi mjasiriamaili kuachwa nyuma katika ushindani wa kibiashara katika soko huria,kwenda na wakati pia kunatoa fursa kwa mjasiriamali kujua njia mpya za uzalishaji. Njia ambazo zinaweza kukusaidia kwenda na wakati ni pamoja na kusoma magazeti,kufanya utafiti,kurambaza katika mitandao mbalimbali.
Endelea kutembelea mtandao wetu tuendelee kujifunza zaidi.

Imeandaliwa na Jerome Mmassy-Arusha,Tanzania.




No comments:

Post a Comment

Featured post

MWANAMKE YAFUATE HAYA; NI MUHIMU KWA MAHUSIANO YAKO

1. Degree yako ya fist class uliyoipata chuo kikuu haiwezi kukufanya uwe mke first class katika ndoa yako bali ni heshima yako na uthubu...