Taarifa fupi toka Mwanahabari Salma Said
Nitaeleza kwa ufupi sana kwa kweli ni unyama na uhuni mkubwa niliofanyiwa ilikuja gari pale airport wakati nikisubiri gari yangu na kuniingiza kwa nguvu katika gari na kunipeleka sehemu wakanifungia na kunipiga sana kisha wanaondoka wanarudi tena wananipiga tena kwa hivyo machungu juu ya machungu maumivu makali sana hawakuwa wanachagua mateke vibao uso ulivimba sana waliponiona pumzi zishanibana nahangaika ndio wakafunga mlango wakatoka nje wakaniacha mpaka asubuhi wakaja tena wakawa wananipiga tu na kusema maneno yao ya vitisho kumbe kosa langu kubwa ni kuandika habari za Mazombi wakinambia najifanya mwandishi na mtetezi wa haki za wanyonge huku wakinipiga na kuniahidi hawataniachia mpaka Dk Shein atakapotangazwa, Na jana ndio wakanirejesha kule kule waliponichukua karibu na kituo cha Taxi cha airport wakiwa wamenifunika uso na kunitupa tu saa 11.30 Alfajiri nilipojifunua ndio nikajikuta nipo hapo nikajiburura hadi kituoni nikaongea na mama mmoja hapo anisaidie akanambia kaa chini mwangu akawa ananiliwaza ndio baadae nikachukua taxi kwenda Aga khan hospitali daktari wangu hakuwepo ikabidi niende Regence Hospitali tokea asubuhi hadi hiyo saa 10 alipokuja Onesmo kunichukua na kwenda polisi kuweka taarifa na kuhojiwa hadi saa 4 usiku. Simu yangu muda mwingi nilikuwa nayo mwenyewe na ndio siku ya mwanzo nilipoongea walipikuja wakanipiga sana sana na muda mwingine simu wakaizima ila hawakuichukua na hawajachukua chochote kwa kuwa walisema shida yao nisiripoti uchaguzi tu
0777 Namba ya Salma Saidi Mwanahabari alietekwa Na kuteswa.
No comments:
Post a Comment