Sunday, 28 February 2016

IMENIFUNDISHA SANA HII STORI USIPITE BILA KUISOMA UTAPATA KITU


Kijana asiye na kazi aitwaye Nolesy aliamua
kumwoa rafiki yake wa muda mrefu
aliyekuwa
akifanya kazi katika benki moja mashuhuri.
Nolesy alijitosa katika ndoa licha ya hofu na
ushauri mwingi aliopewa na ndugu kuwa ni
vibaya kuoa ukiwa huna kazi.
Kila mwezi yule binti alimpa mmewe
mshahara
wake wote wa 800,000 baada ya kutoa fungu
la
kumi kwa ajili ya kanisani.
Nolesy yeye alitoa 200,000 na kumpa mkewe
kwa ajili ya matumizi binafsi na zilizobaki
kijana aliamua atumie kwa matumizi gani. Na
hali hiyo ilidumu kwa miaka mitatu
mfululizo.
Furaha na amani viliitawala nyumba ile na
kwa
wanandoa wale pia kwa miaka mitatu pamoja
na kuwa marafiki wengi wa yule dada
walimfuata na kumwambia huwezi ukawa
unalipa bill zote za nyumba na kufanya kazi
zote wewe tuu na mmeo kakaa tuu kwa nini
msiachane?
Kuna mwezi mmoja kijana yule alitumia zaidi
ya 500,000 akizunguka mikoa mbalimbali kwa
ajili ya intavyuu za kazi.
Hatimaye kijana alifanikiwa kupata kazi
Mbeya
katika kampuni ya Green Entertainments na
kuwa meneja mkuu huku akipokea mshahara
wa milioni tatu na nusu kama kianzio.
Akanunua gari yake ya kwanza mpyaa kwa bei
ya shilingi 18M na akampa funguo mkewe na
kuendelea kutumia usafiri wa daladala kwa
zaidi ya miaka miwili.
Baada ya hapo akanunua gari la pili jipya
lenye
thamani ya 30M na kumpa mkewe na
kulichukua gari la zamani na kulitumia yeye
na
mpya kumpa mkewe.Miaka michache baadae
wakahamia kwenye nyumba yao.
Siku moja mke alikuwa akitafuta dokyumenti
zake katika makabrasha mbalimbali pale
chumbani kwao, alishangazwa kuona kuna
bahasha ndogo imefichwa na ndani kuna
picha
yake wakati wa harusi na akaona kuna
dokyumenti nyingine za manunuzi kiwanja na
magari na vyote vikiwa vimeandikwa kwa jina
lake kabla ya kuona maandishi yaliyoandikwa:
''MKE WANGU NI KILA KITU KWANGU.
ALIKUBALI KUOLEWA NA MIMI NIKIWA SINA
KITU, NA SASA NAAMINI HATA NIKIWA NA
VITU VYOTE NI VYAKE KWANI MOYO WAKE NI
ZAIDI YA KILA KITU KWANGU NA FAMILIA
YETU.AISHI MILELE"
Machozi yalimtoka dada yule na alifurahia
sana
ujumbe ule kabla ya kukumbuka kuwa wiki
chache baadae ilikuwa ni kumbukumbu ya
miaka yao ya ndoa.
Hivi sasa MUNGU amewabariki na wana
watoto
wawili wakike na wakiume na wanapendana
mara mia zaidi ya mwanzo.
Jamani mapenzi ya kweli yapo mpaka sasa.
Je una uhakika kuwa mapenzi uliyonayo kwa
mwenza wako ni sawa au yanaweza
kulinganishwa na haya?
Pamoja na vyote lakini kumbuka
mnachaguana
ili kuishi kwa shida na raha na haijalishi nani
ananunua mahitaji ya nyumbani au kulipa bili
kwa sasa.........


HAKUNA HALI  INAYODUMU MILELE

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgfpnYlr8B79B5gqWk5iu63TR_u8MEUOLlwjH3DrcFpxRzmqLoA6oQiMzW1jCQoMCnYDnPdfVr-VJpvsOHswv32pY1QwWXgpNSA2Tp-Wa3H9tVmyRo0iWJccDmcHQGrBNGN6czLFxKZyBM/s320/D.jpg


No comments:

Post a Comment

Featured post

MWANAMKE YAFUATE HAYA; NI MUHIMU KWA MAHUSIANO YAKO

1. Degree yako ya fist class uliyoipata chuo kikuu haiwezi kukufanya uwe mke first class katika ndoa yako bali ni heshima yako na uthubu...