Monday, 13 June 2016

UMEMPATA “SUGAR DADDY” ANAKULIPIA KODI? HIZI NI SHERIA LAZIMA UZIFUATE!!




Kumekuwa na mikasa kwa Wanaume ambao wanalipiwa kodi na Wapenzi wao wakike kwamba ni mabwege au watoto wa mama kama wengi walivyozoea kuwaita. Lakini kwa upande mwingine kuna wale Wanawake ambao japo sio kwamba hawana kipato kabisa ila wanaamini kuwa wakimpata “Sugar Dady au Sponsor” wa kuwalipia kodi basi fedha yao kidogo waliyonayo wanaweza kuitumia kwenye masuala yao ya Urembo.

Kitu ambacho wanawake hawa wanapaswa kujua ni kuwa, mwanaume anapokulipia kodi kuna sheria au taratibu ambazo aidha kwa kujua au kuto kujua lazima uzifuate. Sheria au taratibu hizo ni hizi;-

Moja, tayari una mahusiano na huyo anayekulipia kodi. Haiwezekani mwanaume akulipie wewe kodi alafu kila siku wewe upo na wanaume wengine labda kama huyo mwanaume ni baba yako mzazi

Pili, mwanaume akikulipia kodi anakuwa na kauli/maamuzi ndani ya nyumba. Akija ataweza anza na kuulizia chakula, yani kama hamna anamaanisha ukapike. Na kwavile wewe ndio unamtegemea basi utakuwa huna namna bali kutimiza anachotaka.

Tatu ni kwamba kiuhalisia hiyo nyumba ni yakwake, sababu anamiliki funguo pia. Na kitendo cha yeye kuwa na funguo inamaanisha kuwa hana haja ya kukupigia simu kuwa anakuja sababu ni kwake. Mtu hana haja ya kupiga simu kwamba anaenda kwake. Anaweza kuja muda wowote atakao. Unaweza ukabadilisha baadhi ya vitu ndani kama vile rangi ya mapazia, ukaweka kapeti jipya ila ni kwake pia.


Nne, kutakuwa na sehemu au kiti maalum ambacho atakuwa anakaa kila mara awapo nyumbani. Na watu wengine walioko nyumbani hawatakuwa wakikaa hilo eneo. Sio kwamba eneo hilo limeandikwa jina hapana, na hiyo ni ishara ya power ndani ya familia. Hii hata zamani ilikuwapo.

Tano hutaweza kuwa kila ukikaa nae basi unaanza kuzungumzia marafiki zako wa kiume, mara ooh mimi na John tumekuwa marafiki kwa muda, Oh John kafanya hiki kafanya kile,hakuna mwanaume anakulipia kodi wewe uje uwafurahishe rafiki zako kwenye nyumba. Tena ukitaka kutoka out na marafiki lazima uombe ruhusa. Kama unaona masharti huwezi get up and pay your rent vinginevyo sharti ndio hilo.

Sita ni kuwa hakuna mwanaume anakulipia kodi kama anajitolea au msaada, kila mtu kuna anategemea faida mwisho wa siku na faida ni kama kufanya mapenzi na mengine. Hapo hana tofauti na mtu ambaye amaewekeza kwenye mradi wake anakaa kusubiria mrejesho. Ukweli ni kuwa ukilipiwa kodi unauza uhuru wako, kinyume chake ni kuwa kama unataka uhuru wako basi lipa kodi yako.

Ila ukweli ni kuwa katika zoezi zima hili la kutegemeana mwisho wa siku kila mmoja anafanikiwa lengo lake. Mwanaume anapata mrejesho wa uwekezaji wake na mwanamke anaweza kununu wigi jipya.

No comments:

Post a Comment

Featured post

MWANAMKE YAFUATE HAYA; NI MUHIMU KWA MAHUSIANO YAKO

1. Degree yako ya fist class uliyoipata chuo kikuu haiwezi kukufanya uwe mke first class katika ndoa yako bali ni heshima yako na uthubu...