Korea Kaskazini imetishia kutekeleza mashambulio ya nyuklia dhidi ya Korea Kusini na Marekani iwapo nchi hizo mbili zitaendelea na mazoezi ya pamoja ya kijeshi.
Mazoezi hayo, ambayo hufanyika kila mwaka, mwaka huu yatashirikisha wanajeshi 300,000.
Serikali ya Korea Kaskazini imetoa taarifa ya ikitishia kutekeleza “shambulio la nyuklia kwa ajili ya haki”.
Ni kawaida kwa Pyongyang kutoa vitisho vya aina hiyo na wataalamu wanatilia shaka uwezo wa Korea Kaskazini kuwa na makombora ya nyuklia.
Hisia hupanda kati ya Korea Kaskazini na Korea Kusini na Marekani kila mazoezi hayo ya pamoja ya kijeshi yanapofanyika.
Pyongyang hutazama mazoezi hayo kama mazoezi ya kujiandaa kuivamia.
Mwaka uliopita, Korea Kaskazini ilitishia kugeuza Washington kuwa “bahari ya moto”.
Wizara ya ulinzi ya Korea Kusini imeionya Pyongyang dhidi ya “hatua za haraka zisizo za busara ambazo zinaweza zikailetea maangamizi”.
CHANZO: BBC SWAHILI
No comments:
Post a Comment